Ni
tukio la aina yake lililojaa kila aina ya ubaguzi wa rangi,ni wiki
iliyopita kijana aliyekuwa akifanya kazi ktk mgodi wa Bulyanhulu wa
Barrick,amefukuzwa kazi baada ya kuonyesha hisia zake kwa binti wa
kihindi raia wa South Africa,ambaye naye ni expart wa mgodi ule.
Walipeana namba za simu,kijana wa watu akatupa ndoana kujaribu bahati
yake,mambo yakamgeuka,binti mbaguzi kashtaki kwa makaburu wa
mgodini,kesi ikaitishwa,hukumu ikatoka kuwa kavunja sheria kwa
kumnyanyasa kimapenzi,kazi ikaisha.
Ajabu ni kuwa weusi huwa wanatongozana lakini hakuna kesi,wala kufukuzwa
kazi lakini baada ya mweusi kumtongoza mweupe,kibao kikageuka kuwa ni
sexual harassment.
Tukio hili limepandisha hasira watu,kwanini mtu abaguliwe ndani ya ardhi
yake na wageni tu tena wenye njaa waliokuja kujistiri kwetu?
Nimeongea kwenye simu na huyu kijana,wiki ijayo naelekea Bulyanhulu ili
kuonana naye nimshawishi aipeleke mahakamani kampuni hii.

0 comments:
Post a Comment