Wednesday, August 6, 2014


Klabu ya Barcelona haisisitizi wala kutoa nafasi ya 'kung'ata' katika mkataba wa Luis Suarez licha ya kuhofia anaweza kung'ata tena, kwa mujibu wa rais wa Barca Josep Maria Bartomeu.
Mshambuliaji wa Uruguay anatumikia adhabu ya kufungiwa miezi minne kutojihusosha na masuala ya soka jambo ambalo litachelewesha kuanza majukumu yake katika klabu hiyo ya Catalan hadi mwezi October baada ya kukutwa na hatia ya kumng'ata mchezaji wa Italia kwenye fainali za Kombe la Dunia - lakini Barca imesema kwamba hiyo haikuwafanya washindwe kukamilisha usajili ta paundi 75million kwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool.
Wakati huo huo Bartomeu amesema tukio la kung'ata linawezakutokea tena - timu ambayo huzingatia kuwa zaidi ya klabu haitoi ruhusa ya makubaliano ya kyng'ata kwenye mikataba na wachezaji wao wapya.




0 comments:

Post a Comment