MTOTO mwenye umri wa miaka tisa (jina linahifadhiwa) anayesoma darasa la tatu katika shule ya msingi Kibaha amenusurika kubakwa na njemba inayofahamika kama Shukuru Abdalahman (49) anayeishi naye nyumba moja, asubuhi ya Julai 31, mwaka huu Kibaha Kwamatias.Akisimulia tukio hilo, mama mzazi wa mtoto huyo, Amina Rashid alisema mtoto wake aliamka asubuhi na kuitwa na Shukuru chumbani kwake kwa madai ya kutaka kumtuma dukani, lakini alipoingia chumbani alifunga mlango na baadaye kumziba mdomo kwa vitambaa kumzuia asipige kelele.
“Baada ya kumtafuta kwa muda, nilikwenda chumbani kwa huyo baba, nikamkuta mwanangu amefungwa vitambaa mdomoni, nilipomuuliza kwa nini hali iko vile, akawa anababaika, nikamchukua mtoto na kumwambia baba yake, tukamuuliza kulikoni, akasema alitaka kuingiliwa kwa ahadi kwamba atapewa chokoleti na hela ya kutumia shuleni.SOMA ZIADI>>
0 comments:
Post a Comment