| Rais wa Marekani Barack Obama amesema majeshi ya Iraq na yale ya Kikurd
yamepiga hatua kubwa kulitwaa tena bwawa muhimu la Mosul kutoka kwa
wapiganaji wa kiislamu kaskazini mwa Iraq.. |
Amesema wamethibitisha kwamba wanauwezo wa kufanya kazi kwa pamoja na
wataendelea kuungwa mkono na majeshi ya Marekani, ambayo tayari
yamefanya mashambulio Zaidi ya anga katika eneo linalokaliwa na
wapiganaji wa kiislamu
Ripoti zinasema kuwa mapambano katika juhudi za kudhibiti maeneo yanayozunguka bwawa hilo yanaendelea.
Katika hatua nyingine kundi la himaya ya
kiislamu linalofanya mashambulizi dhidi ya Wakurd limekanusha kwamba
wapiganaji wake wamepoteza udhibiti wa bwawa hilo.
Wakati huohuo kiongozi wa kanisa katoliki
duniani papa Francis amesema jumuia ya kimataifa itakuwa na haki katika
kuchukua hatua dhidi ya wanamgambo hao
0 comments:
Post a Comment