Wednesday, August 20, 2014

Default NHC: Nyumba 5,000 za bei nafuu kwa wote. Nyumba yangu, Maisha Yangu!

Uliza maswali kadri uwezavyo, NHC watayatolea majibu/ufafanuzi
NHC Website: www.nhctz.com
NHC Facebook: www.facebook.com/nhctz

1. Bombambili - Geita Price (VAT Incl.)


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 43,404,789.60
3 Bedrooms (Faru) 70m2 48,805,059.60
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 48,998,131.20


2. Ilembo - Katavi


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 36,129,240.00
3 Bedrooms (Faru) 70m2 54,341,053.20
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 45,243,748.80




3. Kongwa - Dodoma


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 41,881,244.40
3 Bedrooms (Faru) 70m2 47,006,244.00
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 47,396,210.40




4. Mkinga - Tanga


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 40,703,698.80
3 Bedrooms (Faru) 70m2 46,383,062.40
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 48,200,994.00




5. Mkuzo - Ruvuma


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 42,846,602.40
3 Bedrooms (Faru) 70m2 49,238,992.80
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 52,381,663.20




6. Mlole - Kigoma


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 40,470,483.60
3 Bedrooms (Faru) 70m2 46,052,355.60
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 45,878,400.00




7. Mrara - Manyara


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 42,037,995.60
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 50,515,941.60




8. Mtanda - Lindi


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 39,719,224.80
3 Bedrooms (Faru) 70m2 44,475,285.60
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 47,111,382.00




9. Mvomero - Morogoro


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 40,655,908.80
3 Bedrooms (Faru) 70m2 46,168,963.20
3 Bedrooms (Twiga) 85m2 47,151,525.60




10. Unyankumi - Singida


2 Bedrooms (Nyati) 56m2 49,544,848.80
3 Bedrooms (Faru) 70m2 54,987,174.00

Miliki nyumba yako leo kwa pesa taslimu au kwa mkopo wa nyumba kutoka benki washirika.
Hatua rahisi za kumiliki nyumba yako leo.
  1. Chukua fomu ya kununua Nyumba kutoka ofisi za Shirika zilizopo kwenye mikoa yote au tembelea kwenye tovuti ya Shirika (http://bit.ly/NHChouse)
  2. Rudisha fomu iliyojazwa kikamilifu ikiambatanishwa na uthibitisho wa malipo ya awali ya asilimia kumi (10%) ya thamani ya nyumba unayotarajia kununua (ikiwa na kodi ya ongezeko la thamani yaani VAT).
  3. Maombi yako yatapitiwa kwa umakini ili kuhakikisha kunakuwa na usawa katika uchaguaji wa watu wanaostahili kulingana na vigezo na masharti ya Shirika la Nyumba la Taifa.
  4. Wateja waliokidhi vigezo na masharti, watapatiwa barua za uthibitisho (Letter of Offer), vile vile wateja ambao hawajakidhi vigezo na masharti watafahamishwa kwa njia ya barua.
  5. Mauzo ya nyumba za mradi husika yatafungwa pindi waombaji waliotoa malipo ya awali watafikia asimia mia moja ishirini na tano (125%) ya idadi ya waombaji.
  6. Mteja atapaswa kuthibitisha mpango wa malipo wa asilimia tisini (90%) iliyobakia ya thamani ya nyumba ndani ya kipindi cha siku 90 tangu alipopewa barua ya uthibitisho.
  7. Mteja anaweza kilipia nyumba yake kwa pesa taslimu, malipo ya awamu au kupitia mkopo kutoka benki washirika.
  8. Endapo mteja atashindwa kuthibitisha mpango wa malipo ya kumalizia manunuzi ndani ya siku tisini, Shirika litampatia fursa mteja mwingine kati ya waombaji walioko kwenye orodha ya maombi ya mradi husika (waiting list).
  9. Iwapo mteja atashindwa kukamilisha kulipia malipo ya asilimia tisini (90%) katika kipindi kilichokubaliwa au amelipa asilimia kumi ya awali (10%) akiwa anasubiri (waiting list) na akakosa nyumba, kiasi alichotoa kinaweza kurudishwa au kuhamishiwa kwenye mradi mwingine iwapo mteja atataka kufanya hivyo.
  10. Shirika la Nyumba litafanya utaratibu wa kutafuta hati za nyumba na kisha kuwapatia wanunuzi waliokamilisha malipo ya ununuzi yote.

Attached Thumbnails Attached Thumbnails 

0 comments:

Post a Comment