Tuesday, September 23, 2014



Kama mtakumbuka kuwa baada ya
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe
kutoa maneno ya uchochezi sambamba
na kutangaza maandamano yasiyo na
kikomo nchi nzima kwa kile alichoita
kupinga fedha za walipakodi
kuteketea kwenye Bunge Maalum la
Katiba,

aliitwa Makao Makuu ya jeshi
la Polisi nchini kuhojiwa. Aidha,
wakati Mbowe akihojiwa, viongozi
mbalimbali wa chama hicho ngazi ya
mikoa na wilaya waliandaa maandamano
ambayo hata hivyo hayakufanikiwa.
Cha kushangaza zaidi, mara baada ya
Mbowe kuhojiwa hapo Central Police
na kuona mambo ni magumu kwake,
aliamua kukimbia nchi na kwenda
South Africa ambako hakuna aliyejua
sababu za msingi za kwenda huko.
Halikadhalika, huku Mbowe akitimkia
South Africa, Mbunge wa Arusha
mjini, Godbless Lema kwa niaba ya
viongozi wengine wa CHADEMA nchi
nzima aliwaagiza wafuasi wa chama
hicho kununua mikate ya kutosha na
maji kwa vile wanaenda kwenye
maandamano ambayo hayana kikomo. Pia
aliwaambia wanunue mikeka ili kama
wakihitaji kujipumzisha barabarani
basi waitumie kama matandiko.
Binafsi nimetafakari sana mambo hayo
mawili yaani kuondoka kwa Mbowe na
kauli ya Lema ya kuwataka wafuasi
wao wanunue mikate na maji ya
kutosha. Tafakari yangu imeongezwa
nguvu mara baada ya mjumbe wa Bunge
Maalum la Katiba, Paul Makonda
kutuwekea wazi kuwa kumbe Freeman
Mbowe anagharamia malazi kiasi cha
Dola za Kimarekani 700 kwa siku huko
South Africa. Kiasi hicho ni kikubwa
sana na nimezidi kujawa na
sintofahamu zaidi baada ya kudokezwa
na rafiki yangu ambaye ni kiongozi
wa juu wa CHADEMA kunidokeza kuwa
CHAMA ndo kinagharamia safari hiyo
kwani mwenyekiti wao alisema kuwa
anaenda kwa shughuli za kichama
kumbe anaenda kwenye biashara zake.
Nimejiuliza na nazidi kujiuliza na
nadhani na wenzangu mnajiuliza na
mtazidi kujiuliza, je ni sahihi kwa
Mbowe kukimbia nchi na kwenda
kuponda raha kiasi hicho ilhali
wafuasi wake waliambiwa wanunue
mikate ya kutosha na maji? Nasikia
pia kuwa kudoda kwa maandamano haya
kunatokana na wafuasi wao kukosa
fedha za kutosha kununulia mikate.

0 comments:

Post a Comment