Tuesday, September 9, 2014

Picha Na 2Mshauri wa Mkurugenzi Mtendaji wa Geita Gold Mine katika masuala ya   serikali na jamii Bw. Clement Msalangi (mbele kwa mbali) akielezea mafanikio ya mgodi wa Geita Gold Mine katika utoaji wa huduma bora kwa jamii na uwezeshaji kwa timu ya majaji na sektretarieti iliyofanya ziara katika mgodi huo.
Copy of Picha Na 3Meneja Mahusiano ya Jamii Bw. Manase Ndoloma akisisitiza jambo katika kikao kilichoshirikisha uongozi wa mgodi wa Geita Gold Mine na jopo la majaji na sekretarieti kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji iliyotembelea mgodi huo.
Copy of Picha Na 4Mtaalamu   katika masuala ya mahusiano na maendeleo ya jamii Bw. Joseph Mangilima ( wa pili kutoka kulia) akielezea mchango wa mgodi wa Geita Gold Mine katika mradi wa maji mbele ya bwawa la Nyankanga ambalo maji yake yatasafishwa na kusambazwa kwa wananchi wa Geita kupitia ufadhili wa mgodi huo.
Copy of Picha Na 5Mtaalamu   katika masuala ya mahusiano na maendeleo ya jamii Bw. Joseph Mangilima ( wa kwanza kulia) akitoa maelezo juu ya mchango wa mgodi wa Geita Gold Mine katika ujenzi wa kisima mbele ya timu ya majaji na sekretarieti iliyotembelea mradi huo.Copy of Picha Na 6Afisa Afya Mkuu wa mgodi wa Geita Gold Mine Dkt. Kiva Mvungi ( wa pili kutoka kulia) akielezea mchango wa mgodi wa Geita Gold Mine katika ujenzi wa kituo cha upimaji wa virusi vya Ukimwi na utoaji wa ushauri nasaha cha Geita mbele ya baadhi ya majaji na watendaji wa mgodi huo waliotembelea kituo hicho.
Picha Na 7Meneja Mahusiano ya Jamii Bw. Manase Ndoloma (katikati) akielezea majaji na sekretarieti mchango wa mgodi wa Geita Gold Mine katika ujenzi wa nyumba mpya kwa ajili ya wakazi wa Geita waliohamishwa kwa ajili ya kupisha shughuli za mgodi huo.
Picha Na 8Mtaalamu   katika masuala ya mahusiano na maendeleo ya jamii Bw. Joseph Mangilima ( wa nne kutoka kushoto mstari wa mbele) akiongoza timu ya majaji, sekretarieti na wataalamu wengine kutoka mgodi huo katika ziara kwenye kituo cha watoto yatima cha Moyo wa Huruma, kinachofadhiliwa na mgodi huo.

0 comments:

Post a Comment