Tatizo la ulinzi ndani ya klabu ya Arsenal limeongezeka mara baada ya matabibu wa klabu hiyo kuthibitisha kuwa mlinzi raia wa Ufaransa Mathieu Debuchy kuthibitika kuwa atakua nje ya uwanja kwa takribani miezi mitatu na hivyo kuikosa michezo dhidi ya Chelsea, Liverpool na Manchester United katika kipindi hicho cha miezi mitatu atakachokuwa nje ya uwanja.
Mchezaji huyu wa kimataifa wa Ufaransa aliumia siku timu yake ilipokuwa ikicheza dhidi ya klabu ya Manchester City mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya jumla ya magoli mawili kwa mawili Debuchy aliyenunuliwa kwa paundi milioni 12 kutoka klabu ya Newcastle amefanyiwa upasuaji siku ya ijumaa, upasuaji ambao utamlazimu kukaa nje ya uwanja kwa takribani miezi mitatu.
Michezo ambayo Debuchy atazikosa:
0 comments:
Post a Comment