Tuesday, September 30, 2014

Emmanuel Carlos enzi za uhai wake. Habari kutoka eneo la tukio zinasema kwamba, kwa muda mrefu, marehemu alikuwa na mgogoro usioisha na mkewe Mariamu Suleimani uliosababisha wawili hao kulala katika vyumba tofauti ndani ya nyumba yao. Baadhi ya majirani wa eneo hilo walisema kutokana na ugomvi huo, marehemu alikuwa akirudi nyumbani usiku akiwa amelewa na kumtukana matusi mkewe huku baadhi wakienda mbali na kudai alikuwa haachi hela ya matumizi. 
hali ya kushangaza, mtu mmoja ambaye ni fundi seremala aitwaye Emmanuel Carlos, mkazi wa Kwabinyau Magomeni jijini Dar amekutwa akiwa amejinyonga saa mbili asubuhi Septemba 23, mwaka huu katika kile kinachodaiwa kuchoshwa na mgogoro wa kifamilia.
Hata hivyo, mkewe marehemu anadaiwa kuwa na biashara yake ya samaki na alikuwa akijituma ili kuhakikisha anapata nauli ili arejee nyumbani kwao. 
Mke wa marehehu akilia kwa uzuni. Kwa mujibu wa maelezo yaliyopatikana, mtu wa kwanza kujua kuhusu suala hilo alikuwa ni kijana wake mwenye umri wa miaka saba, Celestine Carlos aliyekwenda chumbani kwa baba yake kuomba hela ya shule, ambapo alimkuta akining’inia kwenye dari baada ya kuwa amejifunga kamba kwenye feni. SOMA ZAIDI>>

0 comments:

Post a Comment