Tuesday, September 9, 2014

indexMahmoud Ahmad Arusha

SERIKALI  kupitia wizara ya habari na utamaduni na michezo imeombwa kushirikiana na taasisi binafsi  kwa kukutanisha makabila  mbalimbali  ili kuondoa chuki binafsi baina ya kabila moja  na makabila mengine.
Tamasha hilo la utamaduni ambalo hufanyika kwa mwaka mara moja  limekutanisha makabila mbalimbali  ambapo makabila hayo waliimba nyimbo zao za asili  zenye jumbe mbalimbali za kuelimisha jamii
Vilevile Tamasha hilo lilifanyika Kijiji cha Haydom wilaya ya Mbulu Mkoa wa Manyara ambapo makabila matano yalikutana  kwa lengo la kuonesha asili zao ambayo ni Wahdhabe, Wadatoga Wairaq,Wamangati pamoja na kikundi cha sangarasasi kutoka Dodoma ,ambapo walijenga nyumba zao za asili  katika kambi hiyo huku wakijipikia vyakula vyao vya asili  ambacho kilikuwa kivutio kikubwa  kwa wageni waliofika katika tamasha hilo.

Pia makabila hayo walicheza mbalumbali kama kurusha mishale ,mchezo wakuchapana na fimbo  pamoja na mashindano ya ngoma  zao za asili  ambapo kila tamaduni walionesha umahiri wake kwa makabila mengine.
Moja ya ngoma zilizotumbuiza ni ngoma ya Sang’arasasi  kutoka Dodoma  ambapo mwenyekiti wa ngoma hiyo  ni bwana Samweli Mandoo ambapo alisema kuwa  kupitia ngoma hiyo  ni njia mojawapo ya ajira tegemezi  kwani wao hufanya shughuli za ujasiriamali kupitia vikundi vyao na kuweza kujikwamua kimaisha .
Aliendelea kusema  kuwa  vijana wanaomaliza elimu  zao na wale ambao hawajamaliza  wanatakiwa kujiunga na vikundi mbalimbali vya utamaduni ili kuweza kudumisha asili yao ya kuzaliwa pamoja na kuweza kuwarithisha asili hiyo watoto wao kwa lengo la kuifanya isipotee.
“tumekuwa tukifanya shughuli hizi hizi kwa kutengeneza vitu mbalimbali kama ngoma ,vinanda mikeka  jambo ambalo limekuwa ninjia nzuri kwetu kujitengenezea ajira na kuacha utegemezi”alisema bwana Mandoo
Mbwana Mandoo aliwataka vijana Kote nchini  kutosubiri ajira kutoka serikalini bali wanaweza  wakajiunga  na vikundi mbalimbali  vya utamaduni ili kuondoa dhana  ya kuajiriwa na kuweza kujiajiri wenyewe na kupunguza wimbi la  vijana wa mitaani.
Kwa upande wake Mratibu wa Tamasha hilo  la Utamaduni Bwana Paulo Amani  alisema kuwa Mtu anayekataa  tamaduni yake ni mfu kwani utanaduni  ndiyo  utambulisho  wa mtu na asili yake katika jamii nyingine,
Bwana Paulo alieleza kuwa Lengo la Tamasha hilo  ni kuleta jamii  za karibu zinazozunguka kijiji cha Haydom  kuja kwa pamoja na kusherehekea  utamaduni wao ambapo walikaa katika kambi hilo kwa muda wa siku tatu.
“Watanzania tumerudi nyuma katika kudumisha tamaduni zetu tumekuwa tukiiga mitindo ya watu kutoka nje jambo ambalo ni kinyume cha maadili na kupoteza asili ya tamaduni zetu”alisema bwana Paulo
Pia aliendelea kusema kuwa Watanzania wanatakiwa kuenzi  utamaduni  wao  na kuacha kuiga  tamaduni za nje  kwani utamaduni wetu ni utalii tosha  ambalo linaweza kuongeza pato la taifa.
Hata hivyo aliitaka serikali kushirikiana na taasisi binafsi  ili kuhakikisha  suala la utamaduni linaheshimiwa na kuthaminiwa ikiwa ni pamoja na kuweka  watu sahihi katika idara husika  wanaoweza kuendesha sekata hiyo kwa umakini.

0 comments:

Post a Comment