Monday, September 8, 2014

DSC_0326
Sam Mapenzi, Joniko Flower na Hashim Donode wakiwapa raha mashabiki wa Skylight Band kwenye Nyama Choma Festival iliyofanyika miwshoni mwa juma katika viwanja vya michezo vya chuo kikuu cha Dar es Salaam.
DSC_0332
Mashabiki wakiwa wameshona kwenye viwanja vya michezo vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Nyama Choma Festival huku Skylight Band wakitoa burudani ya aina yake.
DSC_0010
Aneth Kushaba AK47 akitoa burudani sambamba na Digna Mbepera kwa mashabiki wa muziki wa Live Band kwenye tamasha la Nyama Choma lililofanyika mwishoni mwa juma katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam UDSM.
DSC_0039
Pale Aneth Kushaba AK47 (hayupo pichani) anapogusa mashabiki na uimbaji wake.
DSC_0042
DSC_0034
DSC_0047
Ni hisia tu hakuna kingine....Skylight Band ni balaa.!
DSC_0035
DSC_0071
Aneth Kushaba AK47 akishambulia jukwaa kwenye tamasha la Nyama Choma lililofanyika mwishoni mwa juma kwenye viwanja vya michezo vya Chuo kikuu cha Dar es Salaam.
DSC_0054
 Nyomi la kufa mtu... hapa chezea Skylight Band ndio habari ya mujini kwa sasa.
DSC_0235
DSC_0237
Mashabiki wa Skylight Band wakijiachia kwa raha zao.
DSC_0248
Mmoja wa mashabiki akiwa ameshika kiuno kuhamaki kwa kile anachokiona jukwaani kutoka kwa Skylight Band kwenye tamasha la Nyama Choma.
DSC_0175
Aneth Kushaba AK47 akiwapa vionjo vya aina yake mashabiki wa Skylight Band kwenye tamasha la Nyama Choma.
DSC_0150
Digna Mbepera wa Skylight Band akifanya yake jukwaani kwenye tamasha la Nyama Choma lililofanyika kwenye viwanja vya michezo vya Chuo kikuu cha Dar es Salaam-UDSM mwishoni mwa juma.
DSC_0145
DSC_0337
Sam Mapenzi akiporomosha mistari kwa mashabiki wa Skylight Band Nyama Choma Festival.
DSC_0340
Ni burudani mwanzo mwisho.
DSC_0363
Sony Masamba akiwachizisha mashabiki wa Skylight Band Nyama Choma Festival.
DSC_0188
Mpiga solo wa Skylight Band Allen Kiso Mzuzu akionyesha mbwembwe zake mbele ya camera yetu.
DSC_0189
Wapiga vyombo wa Skylight Band wakiwajibika kuhakikisha mashabiki wanapata kitu roho inapenda.
DSC_0274
Mwanamanyoya akirekodi video clip ya mpiga drums wa Skylight Band Idirsa (hayupo pichani) baada ya kukunwa na upigaji wake.
DSC_0280
Mashabiki wa Skylight Band wakisebeneka na burudani kutoka kwa Sony Masamba na Joniko Flower (hawapo pichani).
DSC_0290
Sony Masamba (kushoto) na Joniko Flower wakishambulia jukwaa huku mpiga gitaa la solo wa Skylight Band Allen Kiso Mzuzu akiwasindikiza wakati wa tamasha la Nyama Choma mwishoni mwa wiki jijini Dar.
DSC_0304
Mwanamanyoya akiwatunza Joniko Flower na Sony Masamba kwenye Nyama Choma Festival iliyofanyika mwishoni mwa juma.
DSC_0255
Pichani juu na chini ni mamia ya mashabiki wa Live Music wakishuhudia burudani kutoka Skylight Band.
DSC_0251
DSC_0218
Mary Lucos akitoa burudani kwa wakazi wa Dar waliofurika kwenye tamasha la Nyama Choma huku akipewa sapoti na Digna Mbepera.
DSC_0223
DSC_0257
DSC_0227
Joshua Ndege (kushoto) akishow love na swahiba wake. 
DSC_0392
Super Model Neema Mbuya aking'ara ndani ya Nyama Choma Festival.
DSC_0394
U-Selfie ulihusika na ripota wako Zainul Photo kutoka viwanja vya michezo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Nyama Choma Festival.
DSC_0095
Hashim Donode wa Skylight Band akishow love na murembo.
DSC_0197
Sam Mapenzi akishow love na mashabiki wake kwenye tamasha la Nyama Choma lililofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar.
DSC_0002
Mdau mkubwa wa Skylight Band Alois Ngonyani akipata ukodak na mai wife wake.
DSC_0004
Alois Ngonyani na mkewe akishow love na marafiki zake waliokuja kushuhudia burudani ya Skylight Band kwenye tamasha la Nyama Choma liliofanyika mapema wikiendi hii kwenye viwanja vya michezo vya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
DSC_0387
Wadau wakisho love na ukodak.
DSC_0401
Rais wa Wanamanyoya na vijana wake wakishow love.

0 comments:

Post a Comment