Monday, September 15, 2014

PIX 1-3
 Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Mhe. Dkt. Pindi Chana akiwahutubia baadhi ya Wabunge Wanawake na Wanaume wakati wa Warsha ya Waheshimiwa Wabunge iliyohusu Kuimarisha Uongozi na kuleta Amani katika Uchaguzi iliyofanyika tarehe 13-14 Septemba 2014 mjini Dodoma.
Na Benedict Liwenga, MAELEZO-DSM.
 
Tanzania imekuwa miongoni mwa Mataifa yaliyoko mstari wa mbele katika kutambua mchango wa mwanamke na kuthamini jitihada zake katika kuleta mafanikio na kuhamasisha mabadiliko ya jamii nzima ili kuhakikisha kuwa usawa wa kijinsia unakuwepo.
 
Kutokana na sifa hiyo, Tanzania imekuwa mfano wa kuigwa Barani Afrika na dunia nzima kwani katika juhudi za kuleta usawa wa kijinsia na kuinua hadhi ya wanawake imefanya jitihada mbalimbali katika nyanja za kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

0 comments:

Post a Comment