ali
ya simanzi imetawala miongoni mwa wakazi wa Makete mjini mkoani Njombe
kufuatia utingo wa lori lililobeba skaveta kugongwa na lori hilo hadi
kufa papo hapo.
Tukio
hilo limetokea jana majira ya saa 11:45 alfajiri wakati lori hilo
likipita kwenye eneo lililolundikwa vifusi kufuatia matengenezo ya
barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Baba mdogo wa marehemu aitwaye Allan Mwalukasa ambaye alikuwepo kwenye lori hilo amesema hata yeye anashangaa kilichopelekea kifo cha ndugu yake kimetokeaje.
amesema Mwalukasa.
Kwa upande wa wananchi waliofika eneo la tukio wamesema marehemu alikuwa akimuongoza dereva namna ya kupitisha lori kwenye vifusi vilivyolundikwa muda mrefu barabarani bila kusambazwa, lakini ghafla aliteleza kwa kuwa alikuwa akipita juu ya vifusi hivyo ndipo alipogongwa na kufariki papo hapo.
Wananchi hao wametupa lawama kutokana na vifusi hivyo kukaa muda mrefu bila kusambazwa hali inayopelekea usumbufu kwa watumiaji wa barabara hiyo, na hivi karibuni mwandishi wetu alizungumza na mkandarasi wa ujenzi huo ambaye alisema amekwenda Morogoro kufuata vifaa vya kumalilisha ujenzi huo.
Hata hivyo wameshauri barabara mbadala zilizojengwa na mkandarasi huyo zitumike ili kuepusha madhara zaidi.
Wananchi hao wametupa lawama kutokana na vifusi hivyo kukaa muda mrefu bila kusambazwa hali inayopelekea usumbufu kwa watumiaji wa barabara hiyo, na hivi karibuni mwandishi wetu alizungumza na mkandarasi wa ujenzi huo ambaye alisema amekwenda Morogoro kufuata vifaa vya kumalilisha ujenzi huo.
Hata hivyo wameshauri barabara mbadala zilizojengwa na mkandarasi huyo zitumike ili kuepusha madhara zaidi.


0 comments:
Post a Comment