Wednesday, October 29, 2014

Msanii wa filamu Bongo, Halima Yahya ‘Davina’. “Mimi sijatafutiwa mume na Bongo Movie, alinitafuta mwenyewe baada ya kuniona kwenye muvi yangu ya Tone la Damu akiwa Italia, sasa nashangaa na ninaumia ninaposikia eti Bongo Movie walinitafutia. MSANII wa filamu Bongo, Halima Yahya ‘Davina’ amesema wanaomsimanga kuwa amepata mume kwa sababu yao hawana hoja kwa sababu Bongo Movie Unity haina ubavu huo.
“Ukweli naombeni mniache kwa sababu hakuna aliyehusika kwa kitu chochote kunikutanisha na mume wangu, hivyo acheni kunisengenya na mimi siringi kwa chochote kama ni kutoka huko kwenye kundi ni maamuzi yangu maana sikuwa naona faida yoyote,” alisema Davina.

0 comments:

Post a Comment