Monday, October 6, 2014

kimemnasa msaidizi wa kazi za ndani (hausigeli) akifanya biashara haramu ya kuuza mwili kwa kisingizio cha mshahara kiduchu.
Kushoto ni hausigeli akifanya biashara ya uchangudoa maeneo ya Sinza jijini Dar.Tukio hilo la aina yake liliingia kwenye kamera za OFM maeneo ya Sinza jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo msichana huyo wa kazi alikutwa kwenye harakati za kusaka wanaume ili kuwapa penzi kwa malipo. Mara baada ya kumnasa na kumlamba picha akiwa na wenzake ambao nao kama yeye walikuwa wamevaa nguo fupi yaani nusu utupu, alianza kuangua kilio hasa alipokuwa akihojiwa kwa nini anajihusisha na biashara hiyo hatarishi katika maisha yake. 

“Jamani mmenipiga picha mtanipotezea kazi yangu, jamani mimi nimeajiriwa, ni mfanyakazi wa ndani kwa mheshimiwa Mikocheni (Dar), nafanya kazi za ndani hii yote ni kujitafutia riziki nje ya kazi,” alilalama binti huyo aliyekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 20 hadi 23.

Baadhi ya machangudoa wakiwa mawindoni.Binti huyo aliwaambia OFM kwamba alifikia hatua hiyo ya kujiingiza katika biashara hiyo ya ngono kutokana na ugumu wa maisha huku lawama akizielekeza kwenye mshahara kidogo wa kazi za ndani.SOMA ZAIDI>>

0 comments:

Post a Comment