Sunday, October 26, 2014

Baba mzazi wa marehemu Focus Saimon (9).Focus aliyekuwa akisoma darasa la tatu katika Shule ya Msingi Kumbukumbu, amedaiwa kufanya tukio hilo Jumamosi iliyopita kwa kufunga gauni la mdogo wake shingoni na kujitundika kwenye komeo hilo mpaka kukata roho. 
Katika hali ya kushangaza, mtoto Focus Saimoni (9), mkazi wa Kwa Bibi Yuda, Kinondoni jijini Dar amekutwa amejinyonga kwenye komeo la mlango wa sebule yao.

Kwa mujibu wa chanzo makini, tukio hilo lilitokea saa 6 mchana wakati wazazi wa mtoto huyo wakiwa kazini na kuacha ufunguo kwa mmiliki wa nyumba aliyejulikana kwa jina la mama Fau.Chanzo hicho kilieleza kuwa siku ya tukio, Focus alirejea nyumbani kutoka shuleni na kumuacha mdogo wake, Irene Steve (5).

Mama mzazi wa Focus Saimoni (kushoto) akihuzunika kumpoteza mwanaye.“Alipofika alichukua ufunguo kwa mama mwenye nyumba na kuingia ndani, akanywa chai. Baada ya muda, mdogo wake (Irene) alirudi na kumkuta tayari ananing’inia kwenye komeo la mlango,” kilisema chanzo. 

0 comments:

Post a Comment