Shukurani Kando (34) ambaye ni mvuvi na mkazi kitongoji cha Kalumo kijiji cha Nambubi, Kata ya Kisorya amejeruhiwa kwa kung’atwa na kiboko na wengine wawili kunusurika wakati wakivua katika Ziwa Victoria wilayani Bunda, Mkoa wa Mara.
“Walikuwa watatu, sasa wakati wakiendelea kuvua ghafla kiboko huyo alitokea na kuanza kuwashambulia na kumjeruhi huyo mmoja, wengine wawili walinusurika baada ya kuogelea hadi nchi kavu,” alisema.
Alisema majeruhi alipelekwa hospitali ya wilaya ya Nansio kutokana na kujeruhiwa vibaya sehemu mbalimbali za mwili wake na hali yake si nzuri.

0 comments:
Post a Comment