Saturday, October 25, 2014

Mtuhumiwa (Mwanaheri) aliyenaswa kwa msala wa utapeli akiwa chini ya ulinzi wa Polisi eneo la Mlimani City jijini Dar.

Mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mwanaheri anadaiwa kunaswa kwa msala wa utapeli na kupewa kashikashi la aina yake baada ya ‘kutaitiwa’ na wanawake wenzake ambao ni wajasiriamali akisemekana kukomba mali zenye gharama za Sh. milioni mbili.Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri Mlimani City jijini Dar, mapema wiki hii, mishale ya saa 10:00 jioni ambapo Mwanaheri aliwekewa mtego na wanawake hao wanaofanyia bishara zao Kariakoo.

Kwa mujibu wa wanawake hao, Mwanaheri alikuwa akiwasumbua kwa muda mrefu bila kurejesha pesa za mali walizompatia katika kikundi chao ambacho kinajishughulisha na kuuza bidhaa za Forever Living.
“Mwanaheri aliingizwa kwenye kikundi na mama yake mdogo (jina kapuni), tukamwamini na kumpatia mzigo wa Sh. milioni mbili.SOMA ZAIDI>>>

0 comments:

Post a Comment