Sunday, October 26, 2014

Singida
JESHI la Polisi mkoani Singida linamtafuta

kijana mmoja mkazi wa Kibaoni katika

manispaa hiyo kwa tuhuma za kumlawiti

mwenzake na kumharibu vibaya sehemu za haja

kubwa baada ya kumnunulia pombe kali aina

ya viroba jogoo tisa.

Kamanda wa polisi mkoani hapa, Geofrey

Kamwela, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi

saa 3:00 usiku eneo la soko la Kibaoni, kata ya

Kindai, na kumtaja mtuhumiwa huyo kwa jina

moja la Athuman.

Alisema kuwa baada ya kila mmoja kumaliza

kunywa viroba vyake, kijana aliyelawitiwa (jina

tunalihifadhi) alimweleza mtuhumiwa kuwa

amelewa kupindukia na hivyo kila mmoja

arejee nyumbani kwao.

“Walipofika eneo la soko la Kindai, muathirika

alimwambia mtuhumiwa amwache hapo ili

apumzike kwa vile pombe ilikuwa imemzidi

sana lakini ghafla alianguka chini na kisha na

kupoteza fahamu,” alisema.

Baada ya muathirika kupoteza fahamu,

mtuhumiwa alitumia fursa hiyo na kuanza

kumwingilia kimwili kinyume cha maumbile.

Alisema kuwa wasamaria wema walimshuhudia

mtuhumiwa akiendelea kufanya unyama huo

dhidi ya rafiki yake lakini walipojaribu

kumkamata, aliwaponyoka na kukimbilia

kusikojulikana.
“Raia wema hao walimbeba muathirika na

kumpeleka nyumbani kwake na baadaye aliweza

kupata fahamu ndipo alianza kusikia maumivu

makali sehemu yake ya haja kubwa,” alisema.

Alisema muathirika alipelekwa hospitali ya

mkoa wa Singida ambako alibainika kuharibiwa

vibaya sehemu zake za haja kubwa.

0 comments:

Post a Comment