MASIKINI! Staa mkali wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja
hivi karibuni amejikuta akiwa katika wakati mgumu na wa hatari kufuatia
watu wasiojulikana kuvamia nyumbani kwake na kutoa onyo kwamba wanampa
siku tano tu za kuishi, Amani lina mkasa kamili.Ishu hiyo ya kushtusha
ilitokea usiku wa saa nane ya kuamkia juzi, Jumanne nyumbani kwa staa
huyo, Sinza Mori jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa chanzo chetu,
watu hao wapatao watatu walitinga nyumbani hapo usiku huo mnene huku
wakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Rav 4 milango mitano rangi ya bluu
ya kuiva na kumkuta mlinzi getini ambaye yupo kwa ajili ya kulinda
usalama wa msanii huyo mwenye maadui kila kukicha.“Walikuwa watano,
walikuwa kwenye Rav 4 milango mitano, rangi ya blue ya kuiva. Wakamkuta
mlinzi, walimuuliza kama Kajala yupo, mlinzi aliwadanganya kwamba
hayupo.”
0 comments:
Post a Comment