MAJANGA! Mwanaume anayedaiwa kuwa na swaga zisizoeleweka, anayejulikana kwa jina moja la Talick, mkazi wa Kinondoni jijini Dar anadaiwa kumchafua Malkia wa Mipasho Bongo, Khadija Omar Kopa kwa kudai kuwa ni mtoto wa kuzaliwa kabisa na muimbaji huyo.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Dully ambaye amekumbana na ushawishi mkubwa kutoka kwa Talick, alisema amekuwa akipata usumbufu mkubwa kutoka jamaa huyo akimuomba urafiki wa karibu akidai hata mama yake (Khadija Kopa) ameshamwambia.

0 comments:
Post a Comment