Thursday, December 4, 2014

HISTORIA YAKE FUPI
Harbinder anatajwa na vyanzo kwamba ni mzaliwa wa Mkoa wa Iringa. Mwaka 1977 akiwa na umri wa miaka 20 ya kuzaliwa na nduguze wawili, Nota Singh na Manjit Singh walianzisha kampuni ya ujenzi wa barabara iliyojulikana kwa jina la Ruaha Concrete Co. Ltd ikitumia SLP 498, Iringa. Ruaha ni sehemu maarufu kwenye Manispaa ya Mji wa Iringa kukiwa na vitongoji vya Ipogoro, Kibwabwa na Ndiuka. Jina la Ruaha linatokana na Mto Ruaha kupita eneo hilo. 

0 comments:

Post a Comment