LEMUTUZ

Thursday, December 4, 2014

MAMA LULU AANGUKIA KWA MZEE WA UPAKO!

Posted by Williammalecela.com on Thursday, December 04, 2014
Mama wa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila.
Mama wa staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila ameangukia katika Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar, linaloongozwa na Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako.’
Chanzo kinasema kuwa mama huyo ameamua kujikita katika maombezi na kwamba hufika kanisani hapo kila siku ya Alhamisi kwa maombezi na siku ya Jumapili kwa ajili ya ibada.
“Ni kweli kila Alhamisi mama yake Lulu huonekana hapa kanisani ambapo hupatiwa huduma ya maombezi kutoka kwa Mzee wa Upako,”
kilisema chanzo.Amani lilifanikiwa kumpata mama Lulu na kumuuliza kama kweli anaabudu katika kanisa hilo ambapo alifunguka;
“Ndiyo nimeamua kumrudia Mungu baada ya kuona watu wanaendelea kutenda dhambi kila siku bila kujali kama mwisho wa dunia upo. Natumia muda mwingi katika kanisa hilo kwa maombezi.”
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

TOTAL PAGEVIEWS

Popular Posts

  • LIVE: RAIS MAGUFULI ANAKABIDHIWA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA MADINI
  • BREAKING NEWZ: BASI LA NGANGA LATUMBUKIA MTARONI KULIKWEPA LORI
  • THE UDAKUZ: WEMA SEPETU Vs WOLPER!!
  • IRAN NA MAREKANI WAZIDI KUIMARISHA UHUSIANO
  • PICHA YA KWANZA YA KANISA LA ASKOFU MTATA GWAJIMA BAADA YA KUKUMBWA NA BOMOA BOMOA YA SERIKALI JANA LIVE.
Copyright © LEMUTUZ

Developed by MKCT