LEMUTUZ

Monday, December 22, 2014

WEMA KORTINI TENA! KIFUNGO KIPO NJE NJE

Posted by Williammalecela.com on Monday, December 22, 2014

Staa wa filamu Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Mkono wa sheria! Achana na drama zake na aliyekuwa mwandani wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, mcheza sinema ‘grade one’ Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ anapandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar kujibu kesi ya kushambuliwa vijana wawili, Rashid Balazi na Juma Bushiri, wakazi wa jijini Dar


HAYUKO PEKE YAKE

Katika kujibu kesi hiyo, Madam Wema hatakuwa peke yake kwani mpambe wake, Petit Man naye anahusika katika kesi hiyo kwa kuwa ndiye mshtakiwa wa kwanza.


Hivi karibuni kabla Madam Wema hajasafiri kwenda nchini Ghana kufanya kazi na staa wa huko, Van Vicker, Petit Man alidaiwa kuhusika kuandaa mchezo mchafu wa kuwateka na kuwashushia kipigo cha mbwa mwitu Rashid na Juma, tukio ambalo lilichukua nafasi nyumbani kwa Wema, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar.
Ilidaiwa kwamba, Petit Man alipoteza simu na kuwahisi vijana hao ambao mmoja wao alikuwa ni fundi bomba, ambaye alikuwa akitengeneza bomba nyumbani hapo.
Mmoja wa vijana walioshambuliwa kwa kipigo nyumbani kwa wema.>>


Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

TOTAL PAGEVIEWS

Popular Posts

  • LIVE: RAIS MAGUFULI ANAKABIDHIWA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA MADINI
  • BREAKING NEWZ: BASI LA NGANGA LATUMBUKIA MTARONI KULIKWEPA LORI
  • THE UDAKUZ: WEMA SEPETU Vs WOLPER!!
  • IRAN NA MAREKANI WAZIDI KUIMARISHA UHUSIANO
  • PICHA YA KWANZA YA KANISA LA ASKOFU MTATA GWAJIMA BAADA YA KUKUMBWA NA BOMOA BOMOA YA SERIKALI JANA LIVE.
Copyright © LEMUTUZ

Developed by MKCT