Friday, January 23, 2015



 
RPC KAGERA HENERY MWAIBAMBE
Kundi la watu wanaodhaniwa ni Majambazi wakiwa na bunduki wameteka Kijiji cha Kimwani katika wilaya ya Muleba Mkoani Kagera kisha kupora mali na kujeruhi watu kwa risasi.

Habari zimesema watu wakadhaa wamelazwa katika hospitali ya Rubya kwa matibabu baada ya kujeruhiwa .

Mwandishi wa harakatinews ameongea na mmoja wa maafisa wa afya katika hospitali ya Rubya na kuelezwa kuwa waliopo katika hospitali hiyo hadi sasa ni watano baada yaw engine 7 kuruhusiwa kutokana na kuwa na majeraha kidogo.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Henery Mwaibambe hakupatikana mara moja baada ya simu yake kuita bila kupokelewa ingawa habari ni kuwa ametuma timu ya makachero katika eneo la tukio.

Tutaendelea kukujuza zaidi juu ya habari hizi

0 comments:

Post a Comment