LEMUTUZ

Thursday, January 1, 2015

PAKA MZEE ZAIDI DUNIANI AMEKUFA

Posted by Williammalecela.com on Thursday, January 01, 2015
http://www.rahatupu.us/
Paka aliyekuwa akitambulika rasmi kuwa ndio mzee zaidi duniani kwa sasa, amefariki dunia akiwa na miaka 24.
Paka huyo aitwaye Poppy alizaliwa mwezi Februari mwaka 1990, mwezi ambao Nelson Mandela alitoka gerezani-, na alitambuliwa rasmi kama paka mkongwe zaidi duniani na rekodi za dunia za Guinness mwezi Mei mwaka huu. 
Alikuwa akiishi mjini Bournemouth, nchini Uingereza. 
Paka huishi kwa wastani miaka 15.
Wataalam wanasema miaka miwili ya mwanzo baada ya kuzaliwa, kwa maisha ya paka ni kama miaka 25 ya binaadam. Baada ya hapo, kila miezi mitatu ya paka, ni kama mwaka mmoja wa binaadam.
Kwa nadharia hiyo, Poppy alikuwa na miaka 114.
Imeripotiwa pia kuwa paka mzee zaidi kuishi duniani alikuwa anaitwa Creampuff, aliyeishi Texas Marekani, ambaye alifika umri wa miaka 38.
Email ThisBlogThis!Share to XShare to Facebook
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

TOTAL PAGEVIEWS

Popular Posts

  • LIVE: RAIS MAGUFULI ANAKABIDHIWA RIPOTI YA UCHUNGUZI WA MADINI
  • BREAKING NEWZ: BASI LA NGANGA LATUMBUKIA MTARONI KULIKWEPA LORI
  • THE UDAKUZ: WEMA SEPETU Vs WOLPER!!
  • IRAN NA MAREKANI WAZIDI KUIMARISHA UHUSIANO
  • PICHA YA KWANZA YA KANISA LA ASKOFU MTATA GWAJIMA BAADA YA KUKUMBWA NA BOMOA BOMOA YA SERIKALI JANA LIVE.
Copyright © LEMUTUZ

Developed by MKCT