Saturday, January 17, 2015

Picha za satelite zinazoonyesha uharibifu katika miiji ya Baga na Doron Baga Kaskazini ya Nigeria
Picha za Satelite za miji ya Nigeria ambayo imesahambuliwa na Boko Haram, zinaonyesha uharibifu mkubwa uliofanyika na kuzua hofu kwamba idadi kubwa ya watu wameuawa na wapiganaji hao.
Taarifa hii ni kwa mujibu wa shirika la Amnesty International.

Picha hizo zinaonyesha zaidi ya nyumba 3,700 zikiwa zimeharibiwa katika miji ya Baga na Doron Baga mwezi huu pekee.
Serikali ya Nigeria imekanusha madai kuwa takriban watu 2,000 waliuawa huku ikisema ni watu 150 pekee waliopoteza maisha.

0 comments:

Post a Comment