Tuesday, February 3, 2015






Bondia Cheka: kama angeelimishwa umuhimu wa kuwa na Wakili, nina imani hadithi ingekuwa tofauti, anaenda Jela, ndio wanatafuta wakili!!
Like ·
  • Leila Omary Kaka kuna kitu nyuma ya pazia kwenyee hii issue.hii nchi Hii??
  • Israel Saria Leila Omary mimi siyo mwanasheria, Ila kwa jinsi ninavyosoma habari za mwenendo wa hukumu, ni kwamba aliambiwa ajitetee na Hakimu, naye akamwambia Hakimu,hana cha kusema, je angekuwa na Wakili si angeshauriwa, sasa utamlaumu nani?
    1 hr · Like · 1
  • Leila Omary Kwani kaka samahani unaposhambulia mtu hamnaga faini ni hukumu tu kaka angu ebu nielekeze sielewi
    1 hr · Like · 1
  • Israel Saria Leila Omary- kwanza kwanini umshambulie mtu?
  • Francis Mkilima Nadhani alilijua hilo labda alikakamaza shingo kuwa ataliweza mwenyewe bila wakili.
    1 hr · Like · 1
  • Shaibu De Ossu Israel Saria Cheka ni mtu mkubwa na ni mtu muhinu ktk taifa hili ni kweli alipaswa kuwa na mwanasheria wake ona sasa anaenda kuzika kipaji chake jela!
    1 hr · Like · 1
  • Hassan Muhiddin Kosa la kushambulia na kudhuru mwili (assault occasioning actual bodily harm) halina faini na adhabu yake ni kifungo cha miaka mitano, kwa mujibu wa sheria za Tanzania. Cheka anapaswa kumshukuru hakimu kwa kuwa "lenient" na kumfunga miaka mitatu tu.
    1 hr · Edited · Like · 4
  • Leila Omary Asante kaka shaibu sikulijua iloo
    1 hr · Like · 1
  • Kambi Abdallah Amestahili kufungwa... Alikuwa na muda wa kutosha kutafuta wakili. Lakini pia proffession yake haimruhusu kupiga/kupigana na watu wasio mabondia. Hilo nalo halijui?
    1 hr · Like · 1
  • Boniventure Wambura Duh..Kumbe alikuwa yeye ndio wakili
    1 hr · Like · 1
  • Israel Saria Leila Omary: alichofanya Cheka ni( GBH) Grievous Bodily Harm) -Really serious harm" alitakiwa tangu mwanzo apate ushauri toka kwa mwanasheria na atumie pesa zake kutafuta unafuu, kwa hapa Uingereza hilo ni kosa kubwa sana, lakini bado narudia kwanini uendekeze hasira. Namsikitikia kwa kutokuwa na washauri wazuri, huku naamini hukumu inaendana na kosa! Pole
    1 hr · Like · 4
  • Leila Omary Kaka Israel Saria nimeelewa Heee!!!!!
    1 hr · Like · 1
  • Mpale Mpoki Saria nakubaliana na wewe kabisa, lakini kumbuka hasira ni human nature, kila binadamu ameumbwa na hasira kumlaumu kwa kuwa na hasira ni kosa. Naomba tulichukulie suala na Cheka kama suala la raia kadhaa ambao wanasimama kizimbani bila kuwa na wakili. ...See More
    1 hr · Like · 2
  • Peter Shundi Mawazo yake yalivyomtuma ndivyo yalivyompoza, this is not a traffic case!
  • Hassan Muhiddin Ni kweli Cheka hakupata ushauri mzuri. Inawezekana alitegemea umaarufu wake ungemsaidia katika kesi hiyo. Hakujua kwamba sheria ikitumika ipasavyo huwa haiangalii umaarufu wa mtu au nafasi yake katika jamii.
    1 hr · Like · 2
  • Mpale Mpoki Israel Saria actually aliambiwa ajiteteee, akasema hana cha kusema, nasoma inaonesha mashihidi wanne waliitwa upande wa mashitaka labda aliamua njia ya tatu ya kujitetea yaani kukaa kimya ambayo inaipa room mahakama kuamua kesi ya kwa inference. Kama u...See More
    1 hr · Like · 4
  • Israel Saria Mpale Mpoki- Asante sana kwa ushauri, na kunielimisha, nilidhani unapokuwa na mafanikio kama hayo ya Cheka, basi suala la kuwa na wakili ni moja kwa moja! Na je alikuwa chini ya kampuni yoyote au alikuwa "solo"?
  • Jovent Johansen Anaweza akakata rufaa tu na hamna namna nyingne nakubaliana nanyi hakuwa na mshauri mzuri na hii ni tabia ya watu wengi maarufu na wenye kipato cha kati, kitu kidogo tu utaskia nitakupoteza kijana unanijua mm ni shida.Kwa hakika mahakama imempa adhabu stahiki.
    1 hr · Like · 1
  • Leila Omary Alipo uko anajuta basi kama tatzo Ni ushauri akitoka kajifunza kitu bahati mbaya ni kwamba nchi za wenzetu ukiwekwa ndani mtu maarufu,umaarufu unazidi coz media zitakulipoti kila muda so ukitoka unakuwa maarufu zaidi ya,,, lakini kwa nchi yetu unazidi kushuka thamani maana media hazina huo muda media zenyewe mpaka uzipe kitu kidogo ndo zilipoti habari zako (NCHI YA KITU KIDOGO)
    1 hr · Like · 1
  • Mbwana Mnose Israel Saria hili ni funzo kubwa sana kwa wanamichezo wetu na hata sisi watu wa kawaida,nadhani kilichomponza CHEKA ni kuishi kwa kujiona yupo juu ya sheria (mfano chenge na kusababisha ajali iliyoua wale wasichana), na pia kuishi kwa kudharau sheria z...See More
  • Mpale Mpoki unajua magazeti yote ya leo hakuna hata moja lililoandika kuhusu the way forward for him Israel Saria sheria inamruhusu kuomba dhamana wakati anasubiri rufaa yake, na wangejua hata jana hiyo hiyo kwa hakimu huyo huyo wangeweza omba dhamana pending appeal. Tunaandika kishabiki zaidi kuliko constructive, kifungu cha 368 cha sheria ya mwenendo wa kesi za jinai CPA
    46 mins · Like · 2
  • Honorary Edward Mallya Role model wake ni Mike Iron Tyson... So anajaribu kumuiga kwa Kila kitu kama Edo alivyosema.... Unless otherwise Inatuonyesha ni jinsi gani Ma staa Wa hapa Nyumbani wapo nyuma. Ishu hiyo ingewezekana kabisa kuishia nje ya Mahakama kwa kumlipa fidia mlalamikaji.
  • Israel Saria Mpale Mpoki msaidieni basi? ( bila kumsahau aliyeumizwa)
  • Honorary Edward Mallya Sasa Mpale Mpoki.. Tatizo ni kwamba hana washauri wazuri. Kama angekuwa nao asingalifikia kifungo. Wasingekubali afungwe Kizembe Kiasi hiki.... Hivi mikataba yake huwa anasainiwa au husaini tu bili kujua content?
    41 mins · Like · 1
  • Ally Bambo Umpa I said the same!!...katka mitigation baada ya kua Convicted,aliulizwa kwanin mahakama isimfunge,akajibu anaiachia mahakama yenyewe!! What a mistake???
    40 mins · Like · 1
  • Mbwana Mnose Kinachoojadiliwa hapa ni ukosefu wa maadili ambao cheka kama kioo cha jamii kaonyesha na hili ni fundisho kubwa sana kwake..hakuna media hasa hawa waandishi wa michezo kama waliweza kufuatilia mlolongo wa maisha yake ya kawaida kabla ya kuwa maarufu unaweza kukuta alichofanya ndio mfumo wa maisha yake.
  • Israel Saria Mpale Mpoki hivi TANZANIA hatuna (Civil Legal Advice (CLA)? Upatapo Shida?
  • Honorary Edward Mallya Na winning point za Appeal hutegemea makosa ya kiufundi na kisheria ktk mwenendo Wa kesi yenyewe. Mpale Mpoki....Do they Exist?
  • Honorary Edward Mallya Zipo nyingi sana Israel Saria na Mororogo ndio inaahika nafasi ya 2 kwa Paralegals nyingi hapa Bongo... Kwa kukosa Ushauri au Kudharau hakufika kupata Msaada Wa Kisheria juu ya Kesi yake.. Je, Wao ndio wangemfuata ilhali yeye anao uwezo Wa kuweka wakili??
  • Israel Saria Honorary Edward Mallya basi hili janga amejitakia!
    22 mins · Like · 1
  • Emmanuel Muga Hivi what happened? Alisema Hana cha kusema wakati wa mitigation au alivyotakiwa ajijitee baada ya prosecution ku rest?
    20 mins · Like · 1
  • Emmanuel Muga Cheka hayuko kwenye category ya watu wanaoatahili msaada wa sheria bure, alipaswa kumwajiri wakili, lakini kuwa na wakili haimaanishi kushinda kesi wakati ushahidi umesimama vizuri unaoonyesha ulifanya kosa@saria
    18 mins · Like · 1
  • Honorary Edward Mallya That is what we can say... Oscar Pistorious pamoja na kuua, Alipambana hadi akafungwa miaka 3 badala ya 15 au Maisha. Hiyo ndiyo thamani ya kuwa maarufu na kujielewa. Kesi ni kujenga hoja thabiti mbele ya Mahakama.
    16 mins · Like · 1
  • Salim Olomi siku zote neno ningejua huja mwisho wa safari.ndio basi tena
  • Israel Saria Emmanuel Muga sasa nini sababu ya kuwa na wakili mzuri? Ni kwamba umefanya kosa, ila unakuwa na wakili mzuri kutafuta mapungufu ya kisheria hatimaye nionekane sina kosa, au nipate adhabu mbadala, ndiyo maana Watu wengi mashuhuri huku Duniani wanatenda makosa, wanaishia kupata adhabu za Kitoto..unanitisha bro! Lol
    13 mins · Like · 2
    • Emmanuel Muga Hapana, kuwa na wakili mzuri maana yake ata exploit vizuri weakness za prosecution, kosa linadhibitishwa bila kuacha Shaka, na kazi ya wakili ni ku punch holes. Kufanyakazi kweli kweli kuhakikisha anajenga mapungufu kwenye kesi ya prosecution. hao wanafanya makosa makubwa halafu wanapata adhabu za kitoto inatokana na mazingira. Pistorious mfano aliua lakini prosecution ikashindwa kudhibitisha mens rea, akapewa adhabu kidogo, marekani yule boss wa Enron mawakili wake hawakumsaidia kutofungwa, Charles Taylor alikuwa anawakilishwa na QC kutoka uk, lakini kashindwa vibaya kesi. Wakili anakusaidia kupata unachostahili kisheria sio kuosha makosa@saria

    1 comment:

    1. Haswaa@wakili Muga. Anachokisema muga ndo sahihi. Wakili kazi yake ni kuraise doubts ambazo zitasaidia kupunguza gravity ya punishment na sio kutakatisha uhalifu.

      ReplyDelete