Katika hali ya kustaajabisha Prof.Tibaijuka wakati akihojiwa na tume ya maadili alipoulizwa swali na Ms Getrude Cyriacus ambaye ni mwanasheria wa tume hiyo juu ya kwanini alitoa pesa hizo benki kwa nyakati tofauti na kwa matumizi tofauti ikiwamo sh. 26 milioni kununua hisa katika benki ya mkombozi wakati huohuo akidai aliomba pesa kwa ajili ya kusaidia shule yake...Alionekana kuchanganywa na swali hilo na kujibu alitoa sh milioni kumi benki kwa ajili ya kununulia familia yake mboga za majani,jibu lililowastaajabisha na kuwaacha hoi watu waliokua wakfuatilia mahojiano hayo yaliyochukua masaa matatu.