![]() |
MWANAMUZIKI
wa kizazi kipya, Suleimani Msindi ‘Afande sele’, ametangaza nia ya
kuwania ubunge wa Morogoro mjini kupitia Chama cha Alliance for Change
and Transparency (ACT-Tanzania).
Msanii huyo ametangaza azma yake hiyo jana mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, baada ya kujiunga na chama hicho akitokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). “Niliumizwa baada ya kusikia kuwa eti katiba ya chama inasema kuwa mwanachama anayekwenda mahakamani kudai haki yake anakuwa amejivua uanachama wake. Kwa chama kama Chadema sikuamini kama kingekuwa na sheria kandamizi kama hiyo ya kuzuia wanachama wake kwenda mahakamani, ambacho ndicho chombo cha mwisho kwa mtu kudai haki,” alisema. Akielezea sababu nyingine iliyomfanya kujitoa Chadema imechangiwa na kuondolewa kwa Zitto Kabwe, ambaye alichangia kumhamasisha kujiunga na chama hicho.
|
Tuesday, March 24, 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)























0 comments:
Post a Comment