Posted by Williammalecela.com on Monday, March 23, 2015
Livingstone Lusinde: Lowassa unahangaika na kupoteza muda kwa sarakasi zako
"Naona
kuna watu wanahangaika na kupoteza mda wao kwnda kujikusanya kwa mtu
wakimuomba achukue fomu ya kugombea uongozi hapa nchini.
Nipende kuwambieni tu kuwa kwanza hizo wazifanyazo ni sarakasi
zinazolenga kuishawishi taasisi yetu ya kisiasa imteue kwa lazima kwa
mantiki kwamba ana ushawishi nje ya taasisi yetu kitu amabcho siyo
kweli, pili ukiangalia kwa upande wa pili watu hao waendapo kwa mtu huyo
hukuta viti, meza, vinywaji na chakula kimeandaliwa kwa ajili yao kitu
ambacho kinaonesha kuwa kuna mpango unafanywa na mtu huyo kuwahadaa Watanzania kuwa wamekuja wenyewe kumbe siyo.
Pili
nipende kuwashauri wanavyuo wa Dodoma waache kujidhalilisha kwa kiasi
hicho walichojidhalilisha leo na kuvivua nguo vyuo watokavyo hapa mjini
Dodoma, mnaacha kusoma na kujikita kwenye utafiti mnatumiwa kwenda
kuvuruga mchakato wa taasisi yetu.
Poleni sana kumbe kusoma sio kuelimika, bora hata mimi mtoto niliyeachwa
yatima toka nikiwa na miaka 4 nikashindwa kupata elimu kwa sababu ya
mazingira magumu ila ninazo akili za kuniongoza na kunionesha jema na
baya."
Chanzo: WALL PAGE @ FACEBOOK LIVINGSTONE LUSINDE
Kilambuzi ale kutokana na uref wakamba yake,mti wenye matunda skuzote ndounaopigwa mawe,hatutaki rais maskini,,muulize yeye aliupata ubunge bila kutumia hata sent5!? Au ni wivu tuu...Lowasaaa juuu..tumien hela nanyie kama mtabahatka kutetea majimbo yenu maana naona maji yashingo
ReplyDelete