NI SHIDA! Msanii wa filamu Bongo, Michael Sangu ‘Mike’ anadaiwa kuipasua ndoa ya muigizaji mwenzake, Halima Yahya ‘Davina’ na mumewe Abdallah Shakoor baada ya kutuhumiwa kutembea na msichana huyo mwenye watoto watatu.
Katika sherehe ya bethidei ya mtoto wao hivi karibuni iliyofanyika katika Hoteli ya Lamada, gazeti hili lilimshuhudia mume huyo akisusa baada ya kugundua kuwa Mike alikuwa ni mmoja wa wasimamizi wa sherehe hiyo.Davina alipotafutwa ili kuzungumzia madai hayo alisema; “Ni kama ulivyoona, ni kweli hakuna maelewano kwenye ndoa yetu, kila ninayefanya naye kazi ananituhumu nina uhusiano naye, Mike ni kiongozi wangu tupo ofisi moja, sasa iliniuma sana alivyoenda kufanya fujo ofisini wakati siyo kweli, namheshimu sana Mike na Thea mkewe ni rafiki yangu siwezi kufanya kitendo kama hicho.”

0 comments:
Post a Comment