Wednesday, April 1, 2015

Kikao kimevunjika muda mfupi uliopita baada ya kutokea vurugu za maneno kufuatia wapinzani kutaka waziri mkuu atoe taarufa juu ya mwenendo wa kura ya maoni ya katiba mpya april 30,2015.kutokana na vurugu hizo za dakika kama 10 hivi spika anna makinda amesitisha gafla shughuli za bunge hadi mchana.

Hali likuwa hivi:

 Mnyika: Nimesimama kupata idhini kwa mujibu wa kanuni ili shughuli za bunge zisitishwe badala yake tujadili zoezi la uandikishaji nchi nzima, mpaka sasa zoezi halijakamilika hata kwa mkoa mmoja tu wa Njome, jambo hili ni la dharura na ilishatolewa na ukaagiza kamati ishughulikie, majibu tupate kikao hiki na leo tunafunga mkutano hamna kitu.

Makinda: Hoja hii inafanana na ile ya kwanza

Mnyika: Amegoma na sauti zimekua nyingi na fujo zimeanza

Makinda: Anang'ang'aniza katibu aendelee na wabunge wa upinzani wamesimama na kutaka majibu kwanza

Katibu: Muswada wa habari

Wabunge: Kwa sauti waliosimama, wanaendelea kupiga kelele wakisema "tunataka majibu..tunataka majibu". tumechoka kuburuzwa..Makinda kwanini unailinda Serikali..Vurugu zimeanza bungeni.

Makinda:Nimesema majibu mtajibiwa baadae

Wabunge: Tunataka sasa hivi kwani Waziri Mkuu yupo

Spika Makinda: Naahirisha bunge hadi jioni.

0 comments:

Post a Comment