Friday, April 17, 2015

AkGlMNL31quEwjijbK6hNLmBMA6Tu8lMMlKH8-vxxbufHii ishu imekuwa kubwa sana kwenye vyombo vya habari, ilianzia Askofu GWAJIMAalipotakiwa kufika Makao Makuu ya Polisi Kanda Maalum Dar kuhojiwa.. ikachukua HEADLINES tena ambapo Askofu huyo aliugua ghafla na kulazwa Hospitali ya TMJ.

Leo imechukua nafasi tena kwenye vyombo vya Habari, moja ya Magazeti ya leo lina kichwa cha habari >>>’Nimechoka kumzungumzia Askofu Gwajima-Kova
DSC01452Kilichoripotiwa muda si mrefu ni kuhusu nyumba ya Askofu huyo iliyopo Mbezi Salasala DAR kuzingirwa na Askari Polisi wakiwa na silaha, waliopo ndani wamegoma kufungua milango.. waumini wake nao wako pembeni wakiwa wanasali na kuimba.
Mwanasheria wake amesema ishu yote ilianzia pale ambapo Askofu Gwajima alitakiwa kuwasilisha nyaraka za vitu anavyomiliki, lakini wao walihitaji kupata barua kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi ili kuwasilisha nyaraka hizo.
Naifuatilia hii kwa ukaribu.. kitakachonifikia nitakusogezea hapa wakati wowote kuanzia sasa.

0 comments:

Post a Comment