Posted by Williammalecela.com on Wednesday, April 22, 2015
Ajali Barabarani: Ni wakati muafaka sasa Serikali iwafukuze Kazi wote wanaohusika na hiyo Sekta
- Leo tena ajali Nzega imeua Mwananchi Mmoja na kujeruhi vibaya
wegine 20, Akili moja ndogo sana huko Serikalini akaamini Kuwalazimisha
Madereva kwenda Shule na kuwalipisha Shillingi Laki Tano ndio jawabu.
Ninasema hivi 95% ya ajali za magari ni PREVENTABLE, nilipokuwa ninasoma
USA nilikuwa ninaendesha 18 Wheel Trucks yaani Malori yenye Matairi 18
nilikuwa na Leseni inayoitwa "Class A" CDL Commercial License ambayo
kuipata ni almost impossible unless una AKILI KUBWA kwa sababu inahitaji
kusoma sana Darasani na Barabarani, halafu hata ukishatimiza masharti
yote bado kuna sharti moja kubwa la mwisho nalo ni once ukiwa na hiyo
Leseni unaitwa "Professional Driver" maana yake ni kwamba ukipatwa na
ajali wakati wowote ule ni your full responsibility unless proven
otherwise by the authorities.
- Madereva wa Mabasi na Malori makubwa ni lazima wawe na Leseni za namna
hii, na ukishafikia hiyo level ya kuwa na hiyo Leseni ni lazima Kampuni
inayokuajiri ijue kabla hujaingia kazini kama umepumzika Masaa 10 toka
ulipoacha kuendesha last na incase Supervisor wako ana wasi wasi haupo
sawa anaruhusiwa na Sheria kukupa kipimo cha Pombe au Drugs kabla ya
kukuruhusu kuingia kazini kuendesha. Serikali kila mwezi inapitia kwenye
Makampuni husika na usafirishaji kutoa Elimu na kuhakikisha Kampuni
zipo sawa na Sheria ya barabarani na usafiri kwa ujumla, wala sio mambo
makubwa sana kuyafanya kuepusha ajali za ajabu ambazo zinaua wananchi
wetu bila sababu ya msingi.
- Mfano mdogo ni Kabla ya Waziri Mwakyembe kushika Wizara ya Uchukuzi,
Bandari ya Dar ilikuwa inaingiza mapato ya Shilling Billioni 40 tu,
likini within mwezi mmoja wa kuishika yeye Mapato yakaongezeka mpaka
Billioni 150 kwa mwezi siku moja nililimuuliza miujiza aliyoifanya
akasema nothing but kuamuru Wateja wote wa Bandari kulipia malipo Benki
tu imetuchukua Miaka 53 ya Uhuru kwa Kiongozi mmoja wa Serikali ya CCM
kufikiria wazo dogo sana kama hilo, Ukweli ni kwamba Bandari yetu
inatakiwa kukusanya Billioni 300 ina maanabado kuna Billioni 150
inayopotelea mikononi mwa wajanja mpaka leo ndio maana hapa mjini
matajiri karibu 90% ni walikuwa wafanyakazi wa Bandarini na TRA, now my
point here ni kwamba hata huko barabarani kinachotakiwa kufanyika wala
sio kitu kikubwa sana kuondoa hizi ajali ila hakuna anayejali maana
tutasikitika siku moja au mbili then tumerudia tulipokuwa inaitwa
Insanity kurudia njia ile ile ukitegemea matokeo tofauti.
- Ninasema umefika wakati wa Serikali ya CCM kuamua kwamba enough na
ajali na kusimamia sheria au kutunga Sheria mpya, inashangaza majuzi
Serikali imetunga Sheria mpya kali za Cyber Crimes lakini sio Sheria
kuhusu ajali barabarani WHY? Kwa sababu habari za mitandao zinawagusa
Wanasiasa ila ajali haziwaguzi sana so ni sawa sawa tu, it is wrong na
ni wakati muafaka wahusika wa hiyo Sekta wakajiuzulu wenyewe au
wafukuzwe kazi, ingawa na sisi wananchi tunahusika sana kwa kuchagua
maviongozi magoi goi kila mwaka haya ndio matokeo yake, wanakuja kwenye
mazishi wanaona huzuni na vilio vyenu lakini hawawezi kwenda Bungeni
kusema lolote kuhusu ajali na vifo vingi vinavyotokea kila siku na ajali
halafu wakija tena kuomba kura mnawapa na kuwafurahia kwa kupewa
pilau!!
- Nchi zote zilizoendelea Duniani zinakuwa na System ya kutafiti
kisayansi Mwaka mzima na mwisho wa Mwaka inatoa maelezo ya chanzo cha
Vifo vingi kwa Taifa kwa ule Mwaka na kuiachia Serikali itafute jawabu,
sisi sijui hata kama tuna chombo kama hicho tungekuwa nacho
isingewezekana tukawa na ajali zote hizi bila jawabu. Jamani enough
Serikali fukuzeni wote wanaohusika na hii sekta cause wameshindwa na ni
wote wahusika tuanze upya kwa kweli hii sekta ni moja ya pungufu kubwa
sana la Serikali ya CCM, ni wakati muafaka wa Serikali kukubali
hadharani huu upungufu na kuufanyia kazi haraka sana kama Sheria
hazitoshi zitungwa haraka lakini haiwezekani tukapoteza wananchi kila
siku na ajali na huku Serikali imekaa kimya sio sawa.
Le Mutuz
0 comments:
Post a Comment