Aliyekuwa kipa wa Arsenal Lukasz Fabianski alifanya kazi ya ziada na kuokoa mashambulizi mengi yaliofanywa na Santi Carzola na Aaron Ramsey huku The Gunners wakilivamia lango la Swansea kama nyuki.
Lakini ikiwa imesalia dakika tano Gomis alipiga kichwa kizuri kilichomwacha kipa wa Arsenal bila Jibu huku teknolojia ya mstari wa goli ikisema kuwa David Ospina aliutoa mpira huo baada ya kupita mstari.
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger baadaye alisema kuwa ushindi huo wa Swansea haukustahili na kwamba timu yake pia haikuwa na bahati.

0 comments:
Post a Comment