MUOGOPENI BAHATI BUKUKU.!
Nimesikitika sana kuusikia wimbo wa Bahati Bukuku aliomuimbia Lowassa na kumpamba kuhusu mbio zake za Urais. Sina tatizo la Lowassa kutafuta Urais maana ni haki yake kikatiba. Ana haki ya kugombea, kupigiwa kura na hata kushinda. Ila nina tatizo na Bukuku aliyeamua kuacha kumuimbia Mungu na kumtukuza mwanadamu.
Nimeainisha makosa 10 ya Bahati Bukuku yanayohusiana na wimbo huo;
1. Bukuku anasema Lowassa atatawala kwa amani na ubora ambao Rais yoyote hataweza kufikia. Hapa kuna makosa mawili. La kwanza ni kusema atatawala.
Nani kamhakikishia Bukuku kuwa Lowassa atatawala? Hivi Bukuku anajua kuwa jina la Lowassa linaweza kupelekwa NEC na lisirudi? Au likarudi halafu wananchi wakamkataa? Sasa yeye anajihakikishiaje kuwa Lowassa atatawala?
2. Pili kasema Lowassa ataongoza kwa ufanisi kuliko wote waliomtangulia na watakaomfuatia. Huu ni ujuha wa kiwango cha "PhD". Hivi unawezaje kupima uwezo wa mtu kabla hajafanya kazi? Ni sawa na kununua nguo za mtoto wa kiume kisa mkeo akiwa na mimba alipenda kula sana ugali, mwishowe anazaliwa wa kike..!
3. Bukuku anasema Lowassa ana hekima kama Suleimani. Hii ni kufuru kubwa kwa Mungu. Maandiko yanasema hakuwahi kutokea mtu mwenye hekima kama Suleimani na hatatokea. Sasa Bukuku kamtoa wapi Lowassa? Ina maana Bukuku ana akili kuliko Mungu aliyeruhusu maandiko hayo?
4. Bukuku anasema Lowassa amepakwa mafuta kama Daudi. Maandiko yanasema Daudi alikuwa Mteule wa Mungu na alipakwa mafuta na Kuhani mkuu Samuel. Kujaribu kumfananisha Lowassa na Daudi ni makosa makubwa. Ni Kuhani gani amempaka mafuta Lowassa? Labda Kuhani Yusuph Makamba.. Na alimpaka mafuta gani? Ya Alizeti au Baby Care.!
5. Si sahihi kwa mtumishi wa kiroho kumfanyia kampeni mgombea waziwazi. Either ni Mchungaji, Padri, Askofu, Sheikh, Ustaadh etc sio sahihi kumsifia mgombea hadharani. Kama unampenda mgombe ibaki moyoni mwako na ufanye maamuzi mwenyewe bila kushawishi wengine.
6. Kumpigia debe mgombea ni kuwagawa waumini. Kuna wafuasi wa Bahati Bukuku hawamkubali Lowassa, sasa haoni anawakwaza?
7. Pia Kuna wafuasi wa Lowassa si Wakristo. Wengine ni waislamu na wengine hawana dini. Sasa Bukuku haoni anawakwaza kwa wimbo wake?
8. Wimbo huu unaibua chuki za kidini na kuonekana Lowassa yupo kwa ajili ya wakristo tu. Kama Lowassa anawapenda pia Waislamu mbona hatujasikia akiimbiwa "Kaswida"? Kumuimbia "mapambio" tu ni ishara ya kuwatenga waislamu na kuwaonesha kuwa Lowassa si mtu wao.
9. Wimbo huu unajenga ushawishi upande mmoja tu wa wakristo. Mbona Waislamu hawakuguswa na wimbo huu? Hivi unawezaje kumshawishi Muumini safi wa kiislamu amkubali Lowassa kwa kusikiliza Pambio??
10. Wimbo huu umemfanya Bukuku kuonekana "Changudoa wa kiroho". Hawezi kuwacheka wanawake wanaouza miili yao kwa fedha, maana na yeye kauza utu wake wa kiroho kwa tamaa ya fedha na mali za dunia.
NB: Kwa ujumla Bukuku amejipunguzia sana heshima yake mbele ya jamii. Waislamu wamemuona ni mdini, wakristo tumemuona mnafiki. Wapo wakristo kadhaa waliojiapiza kutonunua tena kazi zake kutokana na upuuzi alioufanya.
Najua njaa ya pesa ndiyo imemfanya akaamua kuwa vuvuzela la Lowassa. Lakini kwa heshima kubwa aliyokua ameijenga kwenye jamii ni bora asingefanya hiyo kazi. Bora angekubali kukosa hizo hela kuliko upuuzi alioufanya. Njaa ya siku moja haiuwi.
Pesa alizozipata atazitumia na zitaisha lakini doa alilojiwekea halitatoka hata siku anaingia kaburini.
Muasisi wa taaluma ya Public Relations, Arthur Page aliwahi kusema "You may need 20 years to build your reputation, but it takes only 5 seconds to destroy it". Akimaanisha unaweza kutumia miaka 20 kujenga haiba yako mbele ya jamii lakini sekunde 5 tu zinatosha kuharibu kile ulichokijenga kwa miaka 20. Na hivi ndivyo alivyofanya Bahati Bukuku. R.I.P Bukuku.!
Nimesikitika sana kuusikia wimbo wa Bahati Bukuku aliomuimbia Lowassa na kumpamba kuhusu mbio zake za Urais. Sina tatizo la Lowassa kutafuta Urais maana ni haki yake kikatiba. Ana haki ya kugombea, kupigiwa kura na hata kushinda. Ila nina tatizo na Bukuku aliyeamua kuacha kumuimbia Mungu na kumtukuza mwanadamu.
Nimeainisha makosa 10 ya Bahati Bukuku yanayohusiana na wimbo huo;
1. Bukuku anasema Lowassa atatawala kwa amani na ubora ambao Rais yoyote hataweza kufikia. Hapa kuna makosa mawili. La kwanza ni kusema atatawala.
Nani kamhakikishia Bukuku kuwa Lowassa atatawala? Hivi Bukuku anajua kuwa jina la Lowassa linaweza kupelekwa NEC na lisirudi? Au likarudi halafu wananchi wakamkataa? Sasa yeye anajihakikishiaje kuwa Lowassa atatawala?
2. Pili kasema Lowassa ataongoza kwa ufanisi kuliko wote waliomtangulia na watakaomfuatia. Huu ni ujuha wa kiwango cha "PhD". Hivi unawezaje kupima uwezo wa mtu kabla hajafanya kazi? Ni sawa na kununua nguo za mtoto wa kiume kisa mkeo akiwa na mimba alipenda kula sana ugali, mwishowe anazaliwa wa kike..!
3. Bukuku anasema Lowassa ana hekima kama Suleimani. Hii ni kufuru kubwa kwa Mungu. Maandiko yanasema hakuwahi kutokea mtu mwenye hekima kama Suleimani na hatatokea. Sasa Bukuku kamtoa wapi Lowassa? Ina maana Bukuku ana akili kuliko Mungu aliyeruhusu maandiko hayo?
4. Bukuku anasema Lowassa amepakwa mafuta kama Daudi. Maandiko yanasema Daudi alikuwa Mteule wa Mungu na alipakwa mafuta na Kuhani mkuu Samuel. Kujaribu kumfananisha Lowassa na Daudi ni makosa makubwa. Ni Kuhani gani amempaka mafuta Lowassa? Labda Kuhani Yusuph Makamba.. Na alimpaka mafuta gani? Ya Alizeti au Baby Care.!
5. Si sahihi kwa mtumishi wa kiroho kumfanyia kampeni mgombea waziwazi. Either ni Mchungaji, Padri, Askofu, Sheikh, Ustaadh etc sio sahihi kumsifia mgombea hadharani. Kama unampenda mgombe ibaki moyoni mwako na ufanye maamuzi mwenyewe bila kushawishi wengine.
6. Kumpigia debe mgombea ni kuwagawa waumini. Kuna wafuasi wa Bahati Bukuku hawamkubali Lowassa, sasa haoni anawakwaza?
7. Pia Kuna wafuasi wa Lowassa si Wakristo. Wengine ni waislamu na wengine hawana dini. Sasa Bukuku haoni anawakwaza kwa wimbo wake?
8. Wimbo huu unaibua chuki za kidini na kuonekana Lowassa yupo kwa ajili ya wakristo tu. Kama Lowassa anawapenda pia Waislamu mbona hatujasikia akiimbiwa "Kaswida"? Kumuimbia "mapambio" tu ni ishara ya kuwatenga waislamu na kuwaonesha kuwa Lowassa si mtu wao.
9. Wimbo huu unajenga ushawishi upande mmoja tu wa wakristo. Mbona Waislamu hawakuguswa na wimbo huu? Hivi unawezaje kumshawishi Muumini safi wa kiislamu amkubali Lowassa kwa kusikiliza Pambio??
10. Wimbo huu umemfanya Bukuku kuonekana "Changudoa wa kiroho". Hawezi kuwacheka wanawake wanaouza miili yao kwa fedha, maana na yeye kauza utu wake wa kiroho kwa tamaa ya fedha na mali za dunia.
NB: Kwa ujumla Bukuku amejipunguzia sana heshima yake mbele ya jamii. Waislamu wamemuona ni mdini, wakristo tumemuona mnafiki. Wapo wakristo kadhaa waliojiapiza kutonunua tena kazi zake kutokana na upuuzi alioufanya.
Najua njaa ya pesa ndiyo imemfanya akaamua kuwa vuvuzela la Lowassa. Lakini kwa heshima kubwa aliyokua ameijenga kwenye jamii ni bora asingefanya hiyo kazi. Bora angekubali kukosa hizo hela kuliko upuuzi alioufanya. Njaa ya siku moja haiuwi.
Pesa alizozipata atazitumia na zitaisha lakini doa alilojiwekea halitatoka hata siku anaingia kaburini.
Muasisi wa taaluma ya Public Relations, Arthur Page aliwahi kusema "You may need 20 years to build your reputation, but it takes only 5 seconds to destroy it". Akimaanisha unaweza kutumia miaka 20 kujenga haiba yako mbele ya jamii lakini sekunde 5 tu zinatosha kuharibu kile ulichokijenga kwa miaka 20. Na hivi ndivyo alivyofanya Bahati Bukuku. R.I.P Bukuku.!
Babuu Makundi Walaaniwe wamtegemeao mwanadumu na kuabudu miungu mingine isipokuwa Mungu
Nkoswe Mwanalyela Ole Wenu Mzifanyazo Nyumba Za Ibada Kuwa Vichaka Vya Kuficha Maovu Yenu,usifanye Kapeni Za Siasa Ktk Nyumba Ya Ibada.
Erick Mtani Tanzania
ya Leo pesa inanunua utu wa mtu,pesa inanunua mpaka
Maaskofu,Majaji,usishangae hapo hapo hakuna kitu wasanii wetu wa dini
wanaimba lkn hawaishi kweny yale wanayoimba...
Josephat Mwambola ALIYEAMINIKA KUWA NI MTUMISHI WA MUNGU,KAFANYA BIASHARA HARAMU...ANZA KUIMBA TAARABU BAHATI BUKUKU,INJIRI UMEINAJISI
Khadija Lujula huyu n mfanyabiashara
Haji Kipanga Huo
wimbo ni bora mara elfu 10 kusikiliza hata nyimbo za bongo fleva kuliko
huo upuuzi, tena huyo angekua ni muislam alitakiwa acharazwe bakora kwa
kuharibu maandiko ana bahati sana wakristo ni wapole ila kawadhalilisha
walokole kwa huo upuuz, nashauri apuuzwe tu yy na huyo anaemkampenia
Andrew Samson kichwa maji huyo hawezi kupewa rushwa na kupelekwa studio aibu tupu
Mpoki John Poor Bahati, what a shame?
Ntuly Dunga Duh
Goodhelp Mwanginde Bahati bukuku unaharibu neno LA mungu kwa tamaa ya pesa
Goodhelp Mwanginde Bora nisikilize nyimbo za dansi kuliko kusikiliza nyimbo bahati bukuku
Daudi Nyagawa Duu dada heshima yake yapoteya kwasababu yapesa
Profesa MichaelSele Wa San-siro Bahati Bukuku ni mfuasi wa shetani
Johnie M Bentraud Ndo wachumia matumbo wa sikuhizi hao, keshapeww chake ndo anapamba watu kwa mapambio, Mungu hapendi hayo dada bukuku.
Mabula Felix Wacha mungu wanafanya dhambi mpaka shetani anaogopa!!
Happy Katabazi Mwenye mapenzi haoni ingawa macho anayo,ulidhika kuwa nacho japo hakina thamani.
Eliaringa Macha Waimbaji
wa nyimbo za injili kwa sasa ni wakuogopa sana hata maandiko yameandika
na alaaniwe yule amtegemea mwanadamu sasa huyu bukuku haoni kama hii ni
kufuru kwa mola aliye muumba
Eliaringa Macha Anahubiri Injili gani sasa? HUU NI ULIMBUKENI HASWAA WA KUPENDA PESA KULIKO ROHO ZA WENZAKO. R. I. P
Jaqckline S Jordan duu..
Bornface Njechele Wanasiasa wengi, hasa walio waroho wa madaraka na waliolewa UTAMU wa "Keki ya Taifa", aina ya kina #Lowassa,
huwa wanautumia "Upeo Mdogo Wa Watanzania na "Tamaa Ya Pesa" kuwa
mitaji yao katika kuhakikisha wanaendelea kuitafuna nchi, na pengine
hadi ku...See More
Young Fledy Kweli dunian kunawatu ..naviatu
Theobard Zeno Njia moja na mwenzie flora mbasha acha waabike ili wajifunze.
Thankx Goodhope Wale wale hana tofauti na flora mbasha ashinde
Furaha Mwazembe PESA + MUNGU =PESA MUNGU
Moreen Kowi Kowi Wakupewa
Sifa Na Kuabudiwa Ni Mungu Pekee Na Sio Mwanadamu,,kiufupi Bukuku
Hakuwa Na Hofu Ya Mungu Kwani Alisahau Pesa Alizohaidiwa Si Chochote
Angeweza Kuzipata Mara Kumi Yake Kwa Kufanya Kitu Kingne Tofauti Na
Ujinga Huo Ambao Ushakua Upumbavu,
Yohana Mwakisole Hakika
namuogopa bahat bukuku kwa ujinga huu nitumiwa nyimbo nimeisikiliza
mwanzo mwisho. Sasa natangaza yeye pamoja na kazi zake zote sizitaki
tena. Kazi zake zote nikifika nyumban naenda kuzichoma.
Pius Charles bogus sana
Geoffrey Mwaswala Hii
ndo hasara yakuwa na waimbaji wasiojitambua kama uyo bahat yaan
amemsahau Mungu kabisa na kuanza kumtukuza binadam kweli pesa ni habari
nyingne
Maneno Assoly Hiyo ninjaa inamsumbua kamamwezie flora! Inasikitisha sana wanapoteasasa!
Leah Chrissy Mafwenga Siasa
na Mungu ni sawa na mafuta na maji afanye maamuzi aache kusema
anamwimbia Mungu atangaze kua mwimbaji wa Lowasa la sivyo itamgharimu
Leah Chrissy Mafwenga Angeiimba nchi sio mtu kakosea sana
Petro Byamungu Yohana mwakisole nitumie mmojawapo please whatapp
0759586272...See More
0759586272...See More
Buberwa Mwemezi Changamoto kubwa hii
Rabson Mahenge Hayo
ni maono ya mtu, mbona wewe unakosa kazi yake kwa ushabik wa kisiasa ni
nan akuamin wewe kuwa ni mtu mwema na s freemason, yeye kaona bora
Lowassa kitu gan kimekukela hadi ukamtoa hadhalan, sisi tunaompenda
tutaendelea kununua kazi zake na tutaendelea kumsuport
Josephine Kishiwa Tamaa mbaya
Christina Otieno Ni haki yake kusema yaliyomoyon mwake hata kwa ngonjera au nyimbo,,,
Paul Mrema yapo
mengi yatakayotokea kwa huyu lowasa hilo ni jambo dogo sana kumbukeni
shetani ndio ametawala dunia ya sasa sishangai alichofanya huyu bukuku
Side Shalua Nadhan kila mtu ana rais anayemkubali ivo kila mtu atapiga kura atakayepata nyingi ndio rais
Makomemanga Cargo Njaa inatisha binafsi nilimkubali sana huyu dada lakini dah ameniangusha kweli mwanamke hafai kuwa imamu
Paul A Kijuu Ukimwacha Mungu utahangaika sana
Boniphace Mwambapa Duuu
cku za mwisho watu watapenda pesa kuliko kumpenda MUNGU binafsi
cjausikia wimbo huo nisiseme chochote mtoa post urushe huo wimbo
tuusikie
Ebardy Robert Ya mungu apewe mungu na yaliyo ya kaisari apewe kaisari,,, amekosa maadili
Eusebio Mosile hiyi ni hela,inabadilisha kila kitu ukishakubali kutumiwa
Salumu Mpeni Duh! njaa shidaaaaaaaaaaaaah!!!!!!!
Issaya Selemani Torongei Mauna Hayo yote nimaneno kama hamna yakusema jama mlale tu
Sarah William Iyo mwanamke mwenzangu ni njaa
Rajabu Mkungumika Kiukweli
huo wimbo cjausikia hivyo cwezi kuutolea maamuz. Ila bukuku ni
mwinjilisti tena ni mwimbaji Gospal. Lakini ktk nyimbo zake sizioni kama
ni za mungu zaidi naona kama biashara tu. Hivyo namfananisha yeye kama
lady jay dee wa bongo flava. Hivyo kwa mantik hiyo poa ana upeo na haki
yake kama w@sanii wengine.
















































0 comments:
Post a Comment