Tuesday, May 12, 2015


Tetemeko la awali lililotokea tarehe 25 Aprili , lilisajili vipimo vya 7.8.
Madhara ya tetemeko hili hayajabainika ila inasemekana kuwa lilitikisa mji mkuu wa India New Delhi, vilevile mji mkuu wa Bangladesh Dhaka.

Majumba yaliyosazwa na tetemeko la awali katika mji mkuu wa Nepala Kathmandu, yalitikiswa mno na tetemeko hili la hivi punde.
Kulingana na walioshuhudia maelfu ya watu waliokuwa ndani ya majumba yao walitorokea sehemu za wazi hofu ikitanda kuwa madhara na vifo zaidi yatatokea.
''Jamani mungu atuokoe maanake tetemeko hili la hivi punde lilikuwa lakutisha zaidi.
lilikuwa kubwa mno ''anasema Prakash Shilpakar mkaazi wa Kathmandu

Tetemeko hilo lilitokea mwendo wa saa sita adhuhuri saa za Kathmandu.
Kitovu cha tetemeko hilo inadaiwa kuwa takriban kilomita 83km Mashariki mwa Kathmandu, eneo lililoko karibu na mpaka wa China.

0 comments:

Post a Comment