Friday, June 26, 2015


Mbunge wa Mbeya Mjini Mh Joseph Mbilinyi "Sugu" ameamua kulitolea ufafanuzi bungeni suala la kumpeleka mahakamani Mzazi mwenzie ili apewe ridhaa ya kumlea mtoto wao, na hilo limetokana na kujibu kauli ya mbunge Martha Mlata aliyoitoa bungeni jana kuwa kampora mtoto huyo kutoka kwa mama yake

Mh Sugu ameitoa kauli hiyo leo hii Majira ya Saa sita mchana na kusema kuwa anashangazwa na kusikitishwa na kitendo cha Mbunge Martha Mlata kuongelea suala hilo hadharani tena ndani ya ukumbi wa bunge, na kusema yapo mambo ya siri ambayo mtu asingependa yazungumzwe hadharani hasa yale ya mahusiano

"Mh Naibu spika nasikitika sana kwa kitendo hicho cha mbunge Mlata kuzungumzia mambo yangu, lakini hazungumzii ya kwakwe yaliyopelekea ndoa yake kuvunjika, na amekuwa akijitangaza kuwa yeye ni mlokole, sasa ni ulokole upi unakubaliana na mtu anayekiuka maadili kwa kuvaa mavazi yasiyo na maadili ya kitanzania" amesema Sugu

Amesema aliamua kwenda mahakamani kuomba ridhaa ya kumchukua mtoto ili amlee baada ya kuona mzazi mwenzie kuwa hana maadili na amekuwa akivaa nusu uchi na picha zake kusambaa mitandaoni ikiwemo inayomuonesha akiwa amevaa pampasi na nyingine zikimuonesha akiwa amevaa mavazi yanayoonesha nyeti zake picha zilizopigwa kwenye utoaji wa tuzo za Kilimanjaro Music Awards 2015

Amesema kabla ya Martha Mlata kurusha shutuma dhidi yake ni vema angemfuata na kumwambia ili Mh Sugu ampe vithibitisho kabla ya kuweka mambo yake hadharani tena buungeni
Katika hatua nyingine Sugu ameweka wazi kuwa pamoja na mahakama kumpa kibali cha kumchukua mtoto wao kwenye himaya ya mama yake, lakini bado hajamchukua na amesema yeye kama binadamu ameacha suala hilo kwa kuwa linaendelea kupatiwa ufumbuzi kifamilia

Naye naibu spika Job Ndugai amewataka wabunge kuacha kuliongelea tena suala hilo mara baada ya maelezo hayo ya Mbunge Sugu, huku pia akiwaomba waandishi wa habari kuacha kulikuza suala hilo ili kuepusha kumuathiri zaidi mtoto wa Mbunge Sugu na Faiza

0 comments:

Post a Comment