“Cha kushangaza sisi ni kundi lakini hata alipokuwa na sherehe yake juzikati hakutualika kisa kikiwa ni hizo hela, sisi tunamsihi kama mchezo umemshinda arudishe tu hela za watu,” alisema sosi aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Flora alitafutwa kwa njia ya simu ili kuzungumzia tuhuma hizo ambapo alipopatikana alishangazwa na kitendo cha habari hizo kufika gazetini kisha akakata simu.
Mtangazaji Maimartha Jesse ambaye ndiye mweyekiti wa kikundi hicho alipotafutwa kufafanua madai hayo alisema: “Yaani haya mambo hayawahusu kabisa, ni mambo binafsi nawaomba muachane nayo.”
0 comments:
Post a Comment