Monday, June 29, 2015

Diamond Platinums  akiendelea kutoa maelekezo baada ya kuzuiwa na mizigo
KIBANO! Staa wa Bongo Fleva mwenye jina kubwa Afrika, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, juzikati alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya ‘kutaitiwa’ kwa saa mbili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kisa kikiwa wingi wa mabegi (3) makubwa aliyoshuka nayo akitokea nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’, Ijumaa Wikienda linakupa ‘unyunyuz’ kamili.

Staa wa Bongo Fleva Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa ametaharuki.Tukio hilo lililoshuhudiwa hatua kwa hatua na gazeti hili, lilijiri Juni 26, mwaka huu kwenye eneo la kukagulia mizigo ya abiria uwanjani hapo kitendo kilichosababisha Diamond kutokwa na kijasho chembamba.

0 comments:

Post a Comment