Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Said Mecky Sadick akiongea na wanahabari.
Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu (katikati) akiongea na wanahabari baada ya kutembelea kituo hicho.
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
Muonekano wa Kituo cha Stakishari leo mchana, Ukonga jijini Dar.
Askari akiwa katika majukumu yake.
Mkuu wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu alipokuwa akiingia katika kituo hicho.
Gari la mmoja wa marehemu likiwa eneo la tukio.
Moja ya pikipiki ya majambazi hao ikiwa katika kituo hicho.
Wananchi wakiwa eneo la tukio.
MKUU wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu akiambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick wametembelea Kituo cha Polisi cha Stakishari kilichopo eneo la Ukonga jijini Dar kilichovamiwa na watu wanaodaiwa kuwa magaidi na kuua askari wanne jana usiku.
Akiongea na wanahabari kutoka eneo la tukio, IGP Mangu amewataka wananchi kuwa watulivu na kutoa ushiriakiano ili kuwanasa wote waliohusika na tukio hilo la kigaidi ambalo limepoteza maisha ya watu.
Katika tukio hilo askari wanne waliuawa, raia wawili na gaidi mmoja anayedaiwa kuuawa na wenzake.
(PICHA: MAKONGORO OGING’/GPL)
0 comments:
Post a Comment