Wakati
mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF akitarajiwa kuongea na wanahabari
muda mchache ujao kuhusu ushiriki wa chama chake ndani ya umoja wa
katiba ya wananchi UKAWA wanachama mamia wamevamia ofisi za chama hicho
zilizopo hapa hapa BUGURUNI wakiimba nyimbo mbalimbali zakuonyesha kuwa
wanaimani na mwenyekiti huyo ndani ya chama hicho.
Kumekuwa na
sintoifahamu mbalimbali juu ya Chama hicho kujiengua au kubakia ndani ya
muungano huo huku magazeti kadhaa jana yakiriport kuwa mwenyekiti huyo
amejiuzulu nafasi yake ya uenyekiti ndani ya chama hicho kutokana na
shinikizo la wanachama wake.
0 comments:
Post a Comment