WATANZANIA watatu ni miongoni mwa waalikwa wa sherehe za kutimiza miaka 250 ya mafanikio ya kuanzishwa kwa kinywaji maarufu kutoka Ufaransa, Hennessy, sherehe ambayo iliyofanyika Johannesburg, Afrika Kusini hivi karibuni.
Miongoni mwa washiriki hao ambao pia walijumuika katika kuonja kinywaji hicho ni pamoja na; DeogratiusKithamawa East Africa Televisheni, Idris Sultan ambayenimshindimkuuwaonesho la Big Brother Africa 2014 naMpigapicha, pamojana Tanya Mulamula wa kampuni yaStudiored Public Relations ambao walialikwa kuwa sehemu ya uzoefu huo.
Watatu hao walipanda pipa moja kwa moja
hadi Johannesburg ambalo ni jiji lililoteuliwa kama moja ya majiji matano pekee
duniani kuwa mwenyeji wa Hennessy 250 Tour, ambalo ni onesho la sanaa katika
kusherehekea kumbukumbu ya miaka 250 ya kinywaji cha Premium Cognac mwaka huu.
Sherehe hiyo ilichota wageni maarufu ikiwa ni pamoja na
Afisa Mtendaji Mkuu wa Hennessy, Bw. Bernard Peillon; Balozi wa Dunia wa
Hennessy, Maurice Richard Hennessy; mwigizaji na mwimbaji Nandi Mngoma;
mwigizaji Nomzamo Mbatha, Maps Maponyane; mshindi wa BBA 2014 Idris Sultani;
mnyange na aliyekuwa Miss Afrika Kusini, Vanessa Carreira; mwinbaji na mtunzi
wa wa ki-Nigeria, 2Face; DJ wa muziki wa Hip Hop na mfanyabiashara, T-Bo Touch;
mtangazaji wa televisheni, Lorna Maseko-Lukhele, pamoja na mtunzajimwenza wa
tukio hilo na mtaalam wa kumbukumbu za Hennessy, Raphaël Gérard.
Aidha, wageni walialikwa kupata uzoefu wa Hennessy 250
Tour, sambamba na chakula cha jioni na uwasilishaji wa kinywaji cha Hennessy
250 Collector Blend hasa iliyozalishwa na Hennessy Master Blender na Taster
Yann Fillioux kwa ajili ya sherehe hiyo kubwa.
Ikijengwa kwa kampeni ya kisanii ya
Hennessy Artristry iliyozinduliwa mwaka 2014, ziara ya Afrika ya Hennessy 250
Tour inalenga kuwatangaza duniani baadhi ya wasanii wenye vipaji wa Afrika,
kuchanganya mchanganyiko wa sauti kamilifu, uvumbuzi kuona, na kupata uzoefu wa
kipekee, kuzungumzia hasa sanaa mchanganyiko ya Hennessy.
MwenyekitinaAfisaMtendajiMkuuwakampuniya Hennessy, Bernard
Peillon, aliwezakufikakituo cha nneziaraya Hennessy 250 Tour
dunianikotenakufanyakwelikatikajumbazuri la sanaa la Circa Gallery huko
Johannesburg, AfrikaKusini.
Hennessy, ambayonibidhaamaarufuyaKifaransanainayouzikasanaduniani,
inasherehekeakutimizamiaka 250 hukuikiwaimetengeneza chupachacheza
Hennessy 250 Collector Blend –
ambayoimetengenezwakwauangalifumkubwasambambanakufanyiwautafitikwamiaka 4
kablayakuingiasokoni.
Kinywaji cha Hennessy kimerudi mwaka huu kwa ziara
iliyopewa jina la Hennessy 250 Tour; onesho la kusafiri la kisanaa ambalo
litawezesha kutembelea majiji matano makubwa duniani kwa ajili ya
kusherehekea miaka 250 ya ukuu usio na makosa, sanaa mchanganyiko na urithi
wake.
Ziara hiyo imefanyika kwenye maeneo
manne maarufu duniani mwaka huu, ikiwemo miji ya; Guangzhou, Moscow, na New
York, onesho hilo lilitua katika jumba la sanaa lijulikamalo kama Circa Gallery
katika Jiji la Johannesburg Agosti 21, 2015 huku fainali ikifanyika
Jijini Paris, Ufaransa.Mmoja kati ya waalikwa wa ziara hiyo, Tanya, amewataka
watanzania kujiandaa kwa ajili ya Matukio ya Hennessy ambayo yatafanyika hivi
karibuni jijini Dar es Salaam.







0 comments:
Post a Comment