Akizungumzia tukio hilo, kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Kigoma, Shija Ganai ambaye pia ni afisa afya wa mkoa, amesema mkimbizi huyo alianza kuugua akiwa katika kambi ya wakimbizi Nyarugusu na baadaye kupelekwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kigoma baada ya kuugua ugonjwa wenye dalili za ugonjwa huo hasa baada ya kuanza kutokwa damu katika sehemu zote za matundu ya mwili.
Ameeleza kuwa kutokana na hali yake na licha ya kwamba hawajathibitisha kama ameugua ugonjwa wa Ebola, tahadhari zote zimechukuliwa na serikali na mashirika ya afya kimataifa ili kuhakikisha ugonjwa wowote aliokuwa nao hausambai.
Via>>ITV
0 comments:
Post a Comment