
UKAWA HUENDA WAMESHINDWA KABLA HATA HAWAJAANZA …27/8/2015
•Kama ingekuwa ni mechi ya mpira wa mguu, UKAWA
ingefananishwa na timu ambayo kocha dakika za mwisho ameshindwa kuja uwanjani
kutokana na matatizo ya kifamilia. Pia wachezaji wawili wanaotegemewa sana wametolewa
kwa kadi nyekundu. Hivyo timu haina mwongozo na pia ina wachezaji pungufu huku
morali ikiwa ya chini kabisa.
•Mwisho wa kurudisha fomu za kugombea urais na ubunge ilikuwa
ni Ijumaa (21-Aug-2015) na kampeni rasmi zimeanza Jumamosi tarehe 22-Aug-2015 .
•Lakini mpaka sasa kuna dalili 5 kuu zinazoonyesha UKAWA
itashindwa vibaya kwenye kura za urais na ubunge
1. TIMU YA KAMPENI
• Timu ya kampeni ya UKAWA
iliwahitaji sana Dr Wilbroad Slaa (Katibu Mkuu wa CHADEMA) na Prof Ibrahim
Lipumba wa CUF.
• Dr Slaa alihitajika zaidi kwa vile Lowassa ana kazi
mbili kubwa kwenye kampeni. Kwanza ni kujisafisha kwa kashfa za ufisadi na pili
kuelezea nini atafanya ambacho ameshindwa kukifanya kwa miaka mingi aliyokuwa
serikalini katika vyeo tofauti ikiwemo uwaziri mkuu kwamba ni lazima apewe
urais.
• Kwenye suala la kujisafisha, Dr Slaa ndiye aliyekuwa
akihitajika zaidi kumsaidia maana Dr Slaa ndiye aliyekuwa mbeba hoja mkuu ya
kuwapinga mafisadi akiwemo Lowassa aliyemtaja katika “List of Shame” Jumamosi
ya tarehe 15-Sep-2007 katika viwanja vya Mwembeyanga.
• Hawa wawili (Dr Slaa na Prof Lipumba) wamejitoa kwenye
timu wote hawapo kwenye timu. Hii imeleta picha ya UKAWA kutokuwa wamoja na
kuwakilisha kundi kubwa la wanachama ambao hawaafiki Lowassa kujiunga na UKAWA na
kupewa ugombea urais.
• Makada wakuu wengine wa UKAWA
wote watakuwa majimboni kunusuru ubunge. Freeman Mbowe atakuwa jimboni Hai. Tundu
Lissu atakuwa jimboni Singida Mashariki. James Mbatia atakuwa Vunjo. Emmanuel
Makaidi atakuwa Masasi. Godbless Lema atakuwa Arusha Mjini. John Mnyika atakuwa
Kibamba. Lowassa ataachwa na mkiwa.
2. KUSAMBARATIKA KWA MAAFIKIANO
• Umoja wa UKAWA mkoa wa Mara wilaya ya Serengeti
umesambaratika na kila chama (kati ya vyama vi-4) kimesimamisha mgombea wa
ubunge na udiwani kwenye kila kata.
•Jimboni Segerea wana UKAWA watatu wamewakilisha fomu za
kugombea ubunge. Waliowakilisha ni wagombea wawili wa CHADEMA sambamba na
Julius Mtatiro wa CUF.
•Taarifa zinaonyesha, kuna majimbo kama 20 ambayo zaidi
mgombea mmoja wa UKAWA amewakilisha fomu kwa msimamizi wa uchaguzi.
3. WABUNGE WA CCM KUSHINDA BILA KUPINGWA
•Pia kuna majimbo kadhaa ambayo wabunge wa CCM wamepita
bila kupingwa kutokana wagombea kutowarejesha fomu za ugombea ubunge kwa
msimamizi wa uchaguzi au kutokana na kushindwa kwenye mapingamizi.
•Mpaka sasa kuna majimbo ma-4 ambayo CCM wameshinda bila
kupingwa. Majimbo hayo ni Bumbuli, Ludewa, Nanyamba na Mlalo.
4. MAANDAMANO YA KUPINGA WAGOMBEA WALIOPITISHWA
• Maeneo mengi kumekuwa na malalamiko na maandamano
kupinga walioteuliwa kugombea ubunge kwa upendeleo wa uongozi wa juu wakati
walishindwa kwenye kura za maoni.
•Baadhi ya maeneo hayo ni jimbo la Bunda amesimamishwa
Ester Bulaya ambaye alishindwa kwenye kura za maoni.
•Jimboni Kishapu, watu wamepinga uteuzi wa Fred Mpendazoe
kuwa mgombea ubunge.
•Hii ni bila kusahau jimboni Ukonga ambako Mwita Witara
ameteuliwa kugombea ubunge wakati alishindwa kwenye kura za maoni kwa vile tu
ana ukaribu na Freeman Mbowe.
5. UZINDUZI WA KAMPENI WABUMA
• Uzinduzi wa kampeni ilikuwa ufanyike
Jumamosi tarehe 22-Aug-2015
•Uzinduzi wa kampeni ukashindwa kufanyika kwa kisingizio
cha kunyimwa uwanja wa Taifa
•Lakini habari za ndani zinasema uzinduzi ulishindwa
kufanyika kutokana na hali tata na tete ya kiafya ya mgombea urais
• Pia hadi kufikia siku hiyo,
ilani ya uchaguzi ya UKAWA ilikuwa haijaeleweka.
•Badala yake wakaahirisha uzinduzi hadi tarehe
29-Aug-2015 ili waweze kujifunza kutoka kwa CCM.
•Kampeni ya siku 63 sasa itakuwa siku 56. Mabadiliko mabovu
kama haya yanatia wasiwasi kama wana hata ratiba inayoaminika ya mikutano ya
kampeni ya nchi nzima.
THE KING OF ALL BONGO SOCIAL MEDIA NETWORK!!
Le Mutuz Nation
0 comments:
Post a Comment