Monday, September 7, 2015



Katika nchi ya Marekani (kwa mfano wa jambo ninalotaka kulielezea) kuna maeneo ambayo kwenye chaguzi zote huchagua chama cha Republican. Majimbo haya huitwa “stronghold” yaani ngome  ya Republican.


Kuna majimbo ambayo, kwa sababu za kihistoria, karibia chaguzi zote huchagua Democrats. Hii huitwa “stronghold” (ngome)  ya Democrats.

Kuna majimbo ambayo. Haya huitwa “Swing States”. Haya ndio mara nyingi huamua mshindi. Majimbo haya mara nyingi huwa na wapiga kura wanaoitwa “undecided voters”. Kwa majimbo haya, watu wengi hupiga kura kutokana na mazingira ya kisiasa ya mwaka huo.

Nchini Tanzania kuna majimbo na ngome kadhaa kwa jinsi kanda tofauti za mikoa zinavyoweza kugawanywa .

Ili chama kishinde ni lazima kiwe na ngome za kutosha.

Kwa mfano, kila mtu anajua, ngome ya chama cha CUF ipo kwenye eneo dogo sana la Pemba. Hili ni eneo dogo sana. Halitoshi kuleta ushindi. Ndio maana mgombea urais wa CUF, Ubrahim Lipumba mwaka 2010 alipata kura kama 469,780 ambayo haifikii hata idadi ya mabalozi wa shina (mabalozi wa nyumba kumi kumi) wa CCM ambao ni zaidi ya 600,000. Eneo hili dogo la Pemba hivi sasa CUF imepata mshindani mpya ambaye ni ADC.

CUF ni chama chenye wabunge wawili tu Tanzania Bara yaani Lindi Mjini na Kilwa Kusini.

Chama cha NCCR Mageuzi kwa karibia miaka 10 kilikuwa hakina mbunge hata mmoja. Mwaka 2010 kilipata wabunge wa-4 wote kutoka mkoa wa Kigoma pekee. Lakini cha kushangaza, kwenye matokeo ya urais, mgombea urais wa NCCR-Mageuzi, Hashim Rungwe, hakupewa kura nyingi mkoani Kigoma ukifananisha. Kwa hiyo hii sio ngome ya NCCR-Mageuzi. Na mwaka huu, uwepo wa ACT Wazalendo, utaiondoa NCCR Mageuzi kwenye ramani.

Ngome pekee ya UKAWA kwa hivi sasa, ngome ya CHADEMA ambayo ni mikoa ya KASKAZINI kwa maana ya Kilimanjaro na Arusha.

Hii haijatokea kwa bahati mbaya. Hii ina uhusiano mkubwa na asili ya waanzilishi wa chama. Mwenyekiti wa chama, mgombea urais wa chama na wafadhili wakubwa wa chama wote wanatokea ukanda huu.

Watu wote ni mashahidi. Katika kipindi cha miaka mi-5 yaani 2010-2015, matukio mengi ya maandamano na mikutano ya CHADEMA imekuwa ikifanyikia katika jiji la Arusha kuliko sehemu yoyote nyingine ya nchi hii. Mikutano na maandamano haya wakati mwingine imeleta hadi maafa.

Ngome nyingine zote zilizobaki ni za CCM. Katika ngome hizo za CCM, inaweza kutokea sehemu moja moja (hususan mijini) ambako upinzani ukawa maarufu zaidi. Kwa mfano mkoa wa Iringa kunaweza kuwa na kura nyingi za upinzani kutoka Iringa mjini. Lakini ukichukulia ujumla wa mkoa wote na majimbo yake yote, lazima kura nyingi zitakuwa ni za CCM.

 Hizi zote ni ishara ya ushindi wa mapema asubuhi kwa CCM, moja ya vyama vikongwe zaidi barani Afrika.

Le Mutuz Nation

0 comments:

Post a Comment