Tuesday, September 15, 2015

Licha ya wasanii wengi kuhofia kuendelea na ratiba zao za kufanya mambo mbalimbali yahusuyo kazi za sanaa katika kipindi hiki cha uchaguzi, weekend iliyopita Wasanii wanaounda ‘Good Music Family’ wakiwemo Weusi, Navy Kenzo, Jux na Vanessa walifanya show ya pamoja mkoani Mbeya ambayo ilikuwa na muitikio mkubwa.Vanessa Mdee amesema kuwa wao hawaoni sababu ya kuogopa kuendelea kufanya kazi zao hata katika kipindi hiki kwasababu hiyo ndio kazi inayowapa kipato.
“Kusema kweli tunathubutu kufanya show kipindi cha uchaguzi kwasababu kwetu muziki ni ajira ni kazi yetu…Hatuwezi kusitisha kile ambacho kinatuletea mkate,” alisema Vanessa kupitia 255 ya XXL.
Good Music family wakiwa Mbeya
Vee Money hakusita kuwashauri wasanii wengine ambao wamesitisha kufanya kazi zao katika kipindi hiki cha uchaguzi.
“Ningewasihi wasanii wengine wasiogope kufanya vitu katika kipindi hiki kwasababu kama ni ajira yako hutakiwi kuacha kufanya katika kipindi hiki, kitu kikubwa zaidi siku ya kupiga kura wote tuunganike kama Watanzania tukapige kura.”
Kupitia Instagram Jux pia alishare picha na kuonesha kinachoonekana kuwa mavuno ya show ya Mbeya na kuandika:

“Asanteni mbeya kwa upendo wenu #africanboy I ain’t walking for no cheesecake #mbeyamoney #goodmusicfamily we coming to your city soon”

0 comments:

Post a Comment