Friday, October 2, 2015

MWAPACHU - "Namuunga mkono Lowasa, lakini siwezi kuhama CCM kwenda CDM. CDM hawajitambui ila wamempata mwanaume."

SOFIA SIMBA -" Nimefuatwa na vigogo wa CDM wakiniomba niungane nao kuleta mabadiliko, nimewajibu mabadiliko ya kweli yataletwa na Magufuli na si Lowasa. tulifanya makosa makubwa kutoka kikaoni, tuliona dalili za mtu kuandaliwa.. tuliomba msamaha na maisha yanaendelea.. lakini ninachofurahi ule mgomo wetu ulisaidia kuwafanya CCM kuchagua mgombea mwenye sifa."

MWANDOSYA - "Ni kweli nahama.. lakini nahama kutoka Dar kwenda kijijini kwetu Lufilyo Busekelo.. ni kweli CCM walinikwaza lakini siwezi kujidhalilisha kuhamia CDM chama ambacho siku zote nimehubiri kuwa ni wababaishaji."

NCHIMBI - "Nimesoma hizo habari magazetini.. na nimefuatwa na viongozi wa CDM kunibembeleza nihamie kwao.. hivi uanachama mtu anaombwa au anaomba..maajabu ya Dunia ni kutoka chama mathubuti kama CCM na kuhamia Chama kinachoelekea kufa kama Chadema, habari za mimi kuhamia huko ni UZUSHI"

0 comments:

Post a Comment