CHIZIKA!
Wakati hekeheka za maandalizi zikipamba juu ya ndoa ya karne ya staa wa
sinema za Kibongo, Wolper, mwanadada huyo anaonekana kuingiwa na
‘uchizi’ juu ya suala hilo ambapo muda wote anawaza ni kwa namna gani
ataweza kuweka historia juu ya shughuli yake. Akizungumza na Ijumaa
Wikienda, hivi karibuni ndani ya Ukumbi wa Jozi
Village,
jijini Dar, Wolper alisema: “akili haijakaa sawa kabisa, nawaza juu ya
ndoa yangu ambayo muda si mrefu itatimia, silali, sili na sipumui
vizuri, kila kitu kimesimama, ni kama imenitia uchizi, muda wa kuishi na
mwanaume kwenye ndoa takatifu umewadia,” alitiririka Wolper.
Chanzo: GPL

0 comments:
Post a Comment